Wasilisha ombi la tiketi kabla ya Agosti 5 kwa safari za
hadi Novemba 30, 2014
Shirika la Ndege la Emirates, linalosifika
kwa kutoa huduma bora za usafiri wa anga kwa abiria kwa mataifa mbalimbali,
limetangaza ofa maalumu kwa Watanzania watakaokwenda Chicago nchini Marekani,
kupitia Dubai wakitokea Dar es Salaam. Punguzo hilo au ofa hiyo maalumu ni kwa
madaraja ya abiria wa kawaida yaani Economy Class na daraja la wafanyabiashara
‘Business Class’.
Emirates ilitangaza ofa hiyo mapema Februari
mwaka huu na ndege zake zitakuwa zikitua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chicago O’Hare. Safari hizo za kila siku zitaanzia Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Dubai, Terminal 5 ifikapo Agosti 5, 2014 na ndege ya
Emirates itakayotumika ni aina ya Boeing 777-200 LR na hivyo kutoa fursa kwa
Watanzania kutembelea jiji hilo la tatu kwa ukubwa nchini Marekani.
Gharama za tiketi ni kuanzia dola za Marekani
1,309 4,285 kwa tiketi ya daraja la abiria wa kawaida
kwenda na kurudi na kwa abiria wafanyabiashara gharama ya tiketi ni dola za
Marekani 4,285.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa
na Emirates maombi ya ununuzi wa tiketi yafanywe kabla ya Agosti 5 na ununuzi
wa tiketi hizo za ofa utafanywa kati ya Agosti 5 hadi Novemba 30, 2014. Kwa habari zaidi kuhusu
gharama za tiketi na masharti mengineyo, wateja wanaombwa kufuatilia katika
tovuti: http://www.emirates.com/tz.
Chicago iliyopewa hadhi ya jiji tangu mwaka
1837, ina idadi ya watu milioni 2.7na ni jiji linalosifika kwa mambo ya
utamaduni na sanaa mbalimbali. Lakini pia jiji hilo linafahamika kwa kuwa bora
katika michezo na hivyo hivyo kuwavutia watalii wengi kila mwaka. Inakadiriwa
kuwa watalii wanaotembelea jiji hilo kila mwaka ni milioni 46.
Shirika la Ndege Emirates linafanya safari
mbalimbali nchini Marekani na baadhi ya miji ambayo Watanzania wengi
wamefikishwa na shirika hilo ni pamoja na Boston, Dallas Fort Worth, Houston,
Los Angeles, New York City, San Francisco, Seattle na Washington D.C.
Abiria wa
daraja la kawaida, pia wanaweza kununua tiketi kutoka Dar es Salaam kwenda Boston kwa dola za Marekani 1,534, kwenda Dallas Fort Worth 1,519,
Houston 1,518, Los Angeles 1,854, New York City 1,533, San Francisco 1,854,
Seattle 1,854 na Washington D.C dola 1,533. Gharama hizo ni kwenda na kurudi.
Kwa abiria
wanaotaka kusafiri kutoka Dar es Salaam kwa daraja la wafanyabiashara kwenda na
kurudi katika miji ya Marekani, gaharama ya tiketi ni kama ifuatavyo. Kwenda
Boston dola 5,170, Dallas Fort Worth dola 5,810, Houston dola 5,810.
Kwenda Los Angeles ni dola 6,540,
gharama ya New York ni dola 5,170 huku tiketi ya San Francisco ikiuzwa kuanzia
dola 6,540 kwenda Seattle ni dola 6,540 na dola 5,170kwenda Washington D.C.
Emirates ilianza kusafirisha abiria kila siku
kwenda Marekani mwaka 2004 na safari zake ni za moja kutoka Dubai hadi New York
JFK. Kwa sasa safari zake zimepanuka na kuifikia miji ya Washington, Houston,
Dallas, Seattle, San Francisco, Los Angeles. Huduma za kuelekea Chicago
zitazinduliwa Agosti. Wasafiri ni mashuhuda kuwa tuzo ya ubora
wa huduma iliyopewa Emirates inadhihirishwa kwa ubora wa huduma na uzoefu
kutoka kwa wafanyakazi kutoka nchi 120 mbalimbali.
Abiria awapo safarini huburudishwa kwa
aina tofauti za muziki wa kusikiliza na video. Mteja anaweza pia kuomba muziki
autakao kulingana na matakwa yake. Ndege yenye namba EK 725 huondoka Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa kila sikua kuanzia saa 04:50 asubuhi na hutua Uwanja wa Ndege wa
Julius Nyerere saa 09:15 mchana. Ndege hiyo huruka kurejea Dubai saa 10:45
jioni na kuwasili saa 05:20 usiku.

No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269