Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kuvyeka miti wakati wa uzinduzi wa kambi ya Umoja wa Vijana wa CCM, ya mafunzo ya kilimo katika eneo la Boko Timiza, Kibaha mjini mkoa wa Pwani. Katika kambi hiyo vijana wanatarajiwa kufanya mafunzo ya kilimo kwenye shamba la ekari 25.
Kijana akihamasisha vijana wenzake, walioko kwenye kambi hiyo ya mafunzo ya kilimo, eneo la Boko Timiza wilaya ya Kibaha mjini.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizindua jiwe la msingi ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani leo, Septemba 19, 2014. |
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani. Kulia ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Kushoto ni Mbunge wa Kibaha Mjini, Silvestry Koka.
Kinana akipata burudani ya Ngonjera kutoka kwa vijana Chipukizi baada ya kuzindua ujenzi Ofisi ya CCM wilaya ya Kibaha mjini leo. Wapili kulia ni Nape.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimfurahia Chipukizi wa CCM, Suma Iddi, aliyekuwepo wakati akizindua ujenzi Ofisi ya CCM, wilaya ya Kibaha mjini
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akikagua tangi la maji alipokagua ujenzi wa mradi wa maji katika kitongoji cha Muheza, wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Tumbi wilaya ya Kibaha mkoa wa Pwani akimpatia maelezo Katibu Mkuu wa CCM, Kinana kuhusu wodi ya wagonjwa mahututi iliyopo kwa sasa kwenye hospitali hiyo, ambapo alisema bado inahitajika kuwepo dawa za kutosha kuliko ilivyo sasa.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269