Breaking News

Your Ad Spot

Sep 23, 2014

MTEMVU AFANYA MAMBO BUZA

  Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu akiwa anaingia  Ofisi ya katibu kata,ya chama cha Mapinduzi CCM Buza Dar es Salaam .

 Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu akitia saini katika kitabu cha wageni Ofisi ya katibu kata ya chama cha Mapinduzi  CCM Buza Dar es Salaam.

 Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam, Abbas Mtemvu,(wapili kulia) wakipiga makofi wakiimba wimbo wa chama hicho mara alipo wasili Ofisini hapo,kuanzia kushoto ni Mwenyekiti UVCCM kata ya Buza,Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Jimbo la Temeke na msaidizi wa Mbunge wa jimbo hilo upande wa Vijana.Peter Sillo,aliye vaa shati la kijani ni  Mwenyekiti wa CCM kata ya Buza, Shabani Bambo  na wakwanza ni Katibu kata ya Buza Shabani Abdallah.

 Katibu kata ya Buza Shabani Abdallah, akimkaribisha Mgeni rasmi Mbunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu, na akitambulisha  katika hafla fupi ya kukabidhi jezi na pesa taslim kwa  matumizi mbalimbali ya kiofisi, katika moja ya ahadi aliyoitowa kwa majimbo matano kwa wanachama wa chama cha Mapinduzi(CCM) Buza.

 Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Temeke (CCM),Ally Mehalla ,akisalimia wanachama wa chama hicho
 msaidizi wa Mbunge wa jimbo la Temeke upande wa Vijana.Peter Sillo kushoto akisalimia wanachama wa chama cha Mapinduzi (kushoto) Mwenyekiti wa( CCM)  kata ya Buza, Shabani Bambo anaye fatia ni Mbunge wa jimbo la Temeke Abbas Mtemvu na kulia ni Katibu kata ya Buza Shabani Abdallah.

 Viongozi wa Matawi kata ya Buza

 Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu(kulia), akikabidhi Pesa Taslim kwa katibu wa Uchumi wa chama hicho Hawa Zuberi, kwa matumizi mbalimbali ya kata ya Chungu Buza Dar es Salaam.

Mbunge wa jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge Mkoa wa Dar es Salaam Abbas Mtemvu(kulia) akimkabidhi Jezi na pesa taslim katibu wa Tawi la Mashine ya Maji5 Baraka Mohamedi


 Mbunge wa Jimbo la Temeke na Mwenyekiti wa Wabunge  Mkoa wa  Dar es salaam,Abbas Mtemvu (kulia),akimkabidhi Mwenyekiti wa CCM kata ya Buza seti ya Jezi pamoja na Pesa taslim Sh.milioni moja na laki moja.  Johari Mkonde (kushoto), kati ya ahadi aliyoitowa kwa majimbo matano kwa wanachama wa chama cha Mapinduzi . anaye shuhudia ni Mwenyekiti wa chama hicho kata ya buza, Shabani Bambo.



 Mbunge wa Jimbo la Temeke akitoka na viongozi kwanda eneo lililo haribiwa na Mvua na kusababisha njia hiyo kutopitika na Magari yakawa hayapiti katika njia hiyo, kati ya Vituka Machimbo na Buza Shule na jinsikani wataweza kuweka Daraja katika Mto wa Buza ili wanafunzi na wananchi waweze pita kwa urahisi kutokana na ukaribu wa eneo hilo.

 Wakiwa katika kituo kidogo cha Polisi cha Buza ,kujionea maendeleya ya kituo hicho baada ya kutoa Pesa awamu ya kwanza na kuahidi kukimalizia na kuwawekea Fenicha mbalimbali kituoni hapo.
 Njia iliyo haribiwa na Mvua na Gari kuto pita tena

 Mto Buza ulivyo ulivyo haribiwa na Mvua


No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages