4. Mkurugenzi Mtendaji wa na
taasisi ya utafiti wa vyuo vikuu kusini mwa Afrika (ESAURP), Profesa Ted
Maliyamkono akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa kuwajengea uwezo
wajasiriamali wadogo na wakati unaofanywa kwa kushirikiana na FSDT.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mpango wa
Matokeo Makubwa Sasa (BRN), Omari Issa akizindua mradi wa kujengea uwezo
wajasiriamali wadogo na wakati kuhuisha biashara zao ili kupata huduma
za kibenki.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Taasisi
ya Ukuzaji wa Sekta ya Fedha (FSDT), Sosthenes Kewe akizungumza wakati
wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa kuwajengea uwezo wajasiriamali wadogo
na wakati unaofanywa kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti wa vyuo
vikuu kusini mwa Afrika (ESAURP)
wadau wakishuudia uzinduzi huo
……………………………………………….
Na Mwandishi wetu
Zaidi ya wajasiriamali 1500
inchini watafaidika na mradi wa kujenga uwezo wa kibiashara unaolenga
kuimarisha weledi wa kufanya biashara kutoka katika mfumo usio rasimi na
kuelekea kufanya shughuli zao katika mfumo rasmi.
Mradi huo unaofadhiliwa na taasisi ya ukuzaji sekta ya fedha
nchini (FSDT) na kutekelezwa na program ya utafiti ya vyuo vikuu vya
nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika (ESAURP) ni mwendelezo wa mradi
kama huo uliotekelezwa mwaka 2013 na ESAURP ambapo safari hii unalenga
kufikia mikoa kumi ya Arusha, Kilimanajaro, Mbeya, Iringa, Kagera,
Mtwara, Kigoma, Singida, Morogoro, Dodoma.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji wa
ESAURP, Profesa Ted Maliyamkono amesema pamoja na mambo mengine mradi
unalenga kusaidia biashara ndogo na za kati zinazoendeshwa katika mfumo
usio rasimi kupata uwezo na maarifa ya kusaidia kukua na kuwa sekta
rasimi, kupata huduma za kifedha, pia kufahamu benki washirika ili
kutengeneza mabadiliko ya tamaduni za kibenki namna ya kusaidia miradi
ya sekta isiyo rasimi katika miradi inayotafuta huduma za kibenki hasa
mikopo.
“Lengo kuu la mradi ni kujenga uwezo wa biashara ndogo na za
kati zaidi ya 1500 kukua. Jambo ambalo litafanyika kwa kutengeneza
program ya mafunzo inayolenga kusaidia biashara ndogo kushiriki katika
uchumi rasmi” alisema Profesa Maliyamkono.
Mradi pia utatengeneza kada ya wakufunzi wenye uzoefu ambao
watatoa mafunzo ya kukuza ujuzi wa kibiashara kwa biashara ndogondogo
nchi nzima hivyo kuongeza idadi ya huduma za kibiashara nchini na
kupanua uwezo wa maendeleo ya kibiashara nchini.
Akizungumza katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Ufundi wa wa FSDT,
Sosthenes Kewe aliwaambia waandishi wa habari kuwa, taasisi yake
imesaidia mradi huu kwa kuwa unaendana na kazi yao ya kuwezesha
wajasiriamali wadogo na wakati na hivyo kuchangia katika kukuza uchumi,
kutengeneza ajira na kupanua vyanzo vya kodi.
“Biashara ndogondogo na za kati zinanaendelea kutambulika kama
vichocheo muhimu kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo katika nchi za
Afrika. Kama wachangiaji wa pato la vizazi na ajira, kwa hiyo zina
nafasi maalumu ya kukuza sekta binafsi” alisema bwana Omari Issa,
Mkurugenzi Mtendaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa sasa.
Mradi huo unahusisha kujenga mazingira ya kurasimisha biashara
na program ya kujenga uwezo kwa kufanya mafunzo ya siku 5 kwa
wajasiriamali watakaochaguliwa kila mkoa na mafunzo yatakayolenga
• Usimamizi wa biashara,
• Usimamizi wa fedha,
• Kutunza kumbukumbu,
• Kusajiri biashara,
• Masuala ya kodi nk
Mafunzo hayo yatafuatiwa na usimamizi kwa miezi mitatu (ulezi)na
kuandaa vituo vya usaidizi wa kibiashara ambavyo vitafanya kazi kwa
miezi mitatu kwenye mikoa husika.
Mradi huu ni umeanzishwa kwa pamoja FSDT, ESAURP na taasisi shiriki za kifedha nchini.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269