Breaking News

Your Ad Spot

Apr 19, 2015

KINANA ANOGESHA MATEMBEZI YA VIJANA WA JOGING MKOA WA DAR ES SALAAM, LEO

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki matembezi ya Vijana wa Jonging kutoka vikundi zaidi ya 100 kutoka wilaya zote za mkoa wa Dar es Salam, leo, kuanzia Uwanja wa Gonga Majumba Sita  hadi Uwanja wa Social  Sitakishari  Ukonga Dar es Slaam. Matembezi hayo za zaidi ya kilometa sita yaliyokuwa na lengo la kuhamasisha Vijana kujitokeza kupigia Kura Katiba inayopendekezwa, yalipita katika barabara ya Nyerere. Wapili kulia ni Mwenyekiti ws CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhani Madabida na Mwenyekiti wa Mtaa wa Mogo, George Mtambalike
 Kinana akiendelea kuongoza matembezi hayo katika hayo. Watatu kulia ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akionyesha umahiri wa afya yake wakati wa matembezi hayo
 Blogger, Ahmad Michuzi kutoka Michuzi Media, akichuruzikwa na kijasho chembamba wakati akishiriki matembezi hayo ili kupata matukio mbalimbali
 Katibu wa CCM, mkoa wa Dar es Salaam, Abilahi Mihewa, akishiriki matembezi hayo
 Vijana wakihamasika wakati wakiwa katika matembezi hayo katika barabara ya Nyerere
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto), akiendelea na matembezi hayo ya Joging karika barabara ya Nyerere
 Kinana akiwatazama vijana wenye umri mdogo kabisa ambao waliongozana naye katika matembezi hayo
 Licha ya matembezi hayo kuhusisha maelfu ya vijana lakini wasafiri hawakupata usumbufu kutokana na utaratibu kup0angwa vizuri
 Matembezi yakikaribua kuingia kwenye Viwanja vya Social  kumalizia  ngwe ya mwisho
 Vijana wakiyapokea matembezi8 kwa bendera ya taifa kwenye Uwanja wa Social
 Mbunge wa Ukonga, Makongoro Mahanga akimsalimia Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Social mwishoni mwa matembezi hayo
 Vijana wakiselebuka kwenye Vwanja vya Social baada ya matembezi yao kuwsili
 Katibu Mkuu wa CCM akishiriki mazoezi ya viungo baada ya kupo9kea matembezi hayo
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki mazoezi ya viungo baada ya kupokea matembezi ya vijana wa Jogging
 Kijana akisaidiwa baada ya kujisikia vibaya baada ya matembezi
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa katika umati wa Vijana wa Joging baada ya kupokea matembezi ya vijana hao
 Mbunge wa Ukonga Makongoro Mahanga akizungumza mwishoni mwa mapokezi ha Vijana hao wa Joging
Wawakilishi wa Kikundi cha Kaza Roho Sabrina Yasin (kulia) na Herieth Noel wakisoma risala ya kikundi chao kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwenye viwanja vya Social, Sitaki Shari jijini Dar es salaam
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Mogo, George Mtambalike akizungumzia matembezi hayo
 Vijana wa kikundi cha Joging cha Kazaroho, Majumba Sita, Ukonga wakipandisha jukwaani mbuzi kwa ajili ya kunadiwa.


 Msanii maaru kwa jina la msaga sumu akikoleza jukwaa kwa nyimbo zake baada ya matembezi ya vi8jana hao wa Joging

 Vijana wa Yamoto Band wakichangamsha jukwaa kwa burudani baada ya mapokezi ya matembezi ya Vijana wa Joging kwenye Viwanja vya Social
 Katibu wa NEC, Itikadi na U&enezi, Nape Nnauye akizungumza machache na vujana kabla ya Kinana kupanda jukwaani kuwasalimia
 Katibu7 Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana akiwaalimia Vijana walioshiriki matembezi hayo ya Vijana wa Joging
 Vijana wakimshangilia Kinana kwa furaha
 Kinana akimtazama Dogo Aslay wa Yamoto Band wakati akiendelea kutumbuiza baada ya Kinana kuzungumza na Vijana
 Nape akifanya manjonjo yake wakati Yamoto Band wakitumbuiza
 Nape akimsaidia Dogo Alay kusata Jukwaani.
Katibu Mkuu wa CCM, akiruka kutoka jukwaani baada ya kumaliza kusalimia vijana hao wa Jogging
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi vya Joging ambao waliongoza matembezi hayo leo
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na baadhi ya waandshi wa habari mwishoni mwa matembezi hayo. imetayarishwa na theNkoromo Blog

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages