Mhamasishaji kutoka
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester Riwa katikati
akizungumza na Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Monduli Bibi. Rose Mhina
kulia kabla ya kukutana na vijana wa Kata ya Monduli juu na Kata ya Mfereji kutoa
elimu ya ujasiriamali na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana jana, katika Halmashauri ya
Monduli Mkoa wa Arusha. Kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw.
Laurean Masele.
Mhamasishaji kutoka
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester Riwa akitoa mada ya
Ujasiriamali, Ujuzi na Stadi za Maisha kwa vijana wa Kata ya Monduli juu na
Kata ya Mfereji jana katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoa wa Arusha.
Afisa Maendeleo ya
Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga
akiwaelekeza vijana walioudhuria semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha
na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kutoka kata za Monduli juu na Mfereji
Halmashauri ya Wilaya ya Monduli jinsi wanavyotakiwa kuzingatia mwongozo unaosimamia
Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.
Mkuu
wa Kituo cha
Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele akitoa mada ya Uongozi bora
wakati wa
semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya
Vijana jana katika Kata ya Monduli juu Halmashauri ya Wilaya ya Monduli
Mkoa wa Arusha.
Afisa Ushirika kutoka
Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bi. Ester Tarimo akiteta na vijana wa kata ya
Monduli juu na Mfereji namna ya kujiunga na Saccoss kwa maendeleo ya vijana
wakati wa semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo
ya Vijana jana katika Kata ya Monduli juu Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoa
wa Arusha.
Vijana wa Kata za
Monduli juu na Mfereji wakifuatilia kwa makini mafunzo yaliyokuwa yakitolewa
wakati wa semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo
ya Vijana jana katika Kata ya Monduli juu Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoa
wa Arusha.
Mmoja wa washiriki wa
semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana
akichangia wakati wa semina hiyo iliyofanyika jana katika kata ya Monduli juu
Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Mkoa wa Arusha.
Vijana wa Kata za
Monduli juu na Mfereji katika picha ya pamoja na wahamasishaji kutoka Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na wadau wa vijana kutoka Halmashauri ya
Wilaya ya Monduli baada ya kufunga semina ya siku moja iliyofanyika jana katika
Kata ya Monduli juu Halmashauri ya Monduli Mkoa wa Arusha. (Picha zote na Genofeva Matemu – Maelezo Monduli)
Na Genofeva Matemu –
Maelezo Monduli
VIJANA Halmashauri ya
Wilaya ya Monduli Kata za Monduli juu na Mfereji wametakiwa kuwa na miradi ya
mfano inayokopesheka na inayoonekana ili kuweza kupata fedha zinazotolewa na
Mfuko wa Maendeleo ya Vijana unaosimamiwa na Wizara ya Habari, Vijana,
Utamaduni na Michezo.
Rai hiyo imetolewa na
Mhamasishaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Ester
Riwa wakati wa Semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa
Maendeleo ya Vijana iliyofanyika jana katika Kata ya Monduli juu Halmashauri ya
Wilaya ya Monduli Mkoa wa Arusha.
Bibi. Riwa amesema
kuwa jitihada za awali zifanywe na vijana wenyewe kwa kuwa na mwamko
wa kuleta maendeleo yatakayotokana na miradi endelevu na yenye malengo kwani
kwa kufanya hivyo wataweza kukabiliana na hali ya maisha ya sasa na kuwa mfano
katika jamii na Taifa kwa ujumla.
Aidha Afisa Maendeleo
ya Jamii Wilaya ya Monduli Bibi. Rose Mhina amewataka vijana wa Monduli kutokupenda
kubebwa kwa kupewa fedha za bure kwa kununuliwa na wanasiasa bali wazidi kujijengea
mazoea ya kuwekeza na kuchukua mikopo inayotolewa na Serikali kwa vijana yenye
riba nafuu na kurejesha fedha hizo kwa wakati ili vijana wengine waweze
kufikiwa na fursa hiyo.
Akizungumza na vijana
wakati wa semina hiyo Afisa Ushirika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli Bi. Ester
Tarimo amewataka vijana kutokuwa watu wakusukumwa kutafuta maendeleo yao bali
wawajibike na kutafuta fursa zilizopo ili kuweza kuondokana na hali ya
kutegemea kazi moja ya ufugaji wa mifugo.
“Vijana wa Munduli
hamjazaliwa kuishia hapo mlipo, msipende kusukumwa na watu kutafuta maendeleo
yenu changamkieni fursa zilizopo na kuwajibika katika jamii zenu bila ya kuwa
na ubaguzi wa kijinsia kwani Monduli haitakiwi kuwa kama ilivyo kwa sasa”
alisema Bi. Tarimo.
Kwa upande wake
mshiriki wa semina ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa
Maendeleo ya Vijana Bw. Mboyo Kayai amesema kuwa vijana wa Monduli wanaweza
kama watapatiwa elimu ya watu wazima kwani kwa sasa jamii kubwa ya vijana
katika Halmashauri hiyo hawajui kusoma na kuandika kitu kinachowapelekea
kushindwa kuwa na mbinu mbadala za kiujasiriamali.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269