Mashabiki wa Simba wakifuatilia
mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya timu hiyo dhidi ya Mgambo JKT ya
Tanga, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam .
Emmanuel Okwi wa Simba akipiga krosi
kuelekea lango la Mgambo JKT, huku akiangaliwa na Bashiru Chanache wa
Mgambo JKT, wakati wa mchezo huo.
Emmanuel Okwi wa Simba akishangilia
bao lake la tatu aliloifungia timu yake hiyo, wakati wa mchezo huo leo
Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Okwi amefunga mabao 3 kati ya 4
yaliyofungwa katika mchezo huo na kuondoka na mpira.
Emmanuel Okwi (kushoto) wa Simba
akishangilia pamoja na Ibrahim Ajib (katikati) na Said Ndemla moja ya
mabao yake 3 aliyoifungia timu yake hiyo, wakati wa mchezo huo
Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ubao wa matangazo ukionesha Simba mabao 3 na Mgambo JKT ya Tanga 0, wakati wa mapumziko ya mchezo huo.
Ibrahim Ajib, akiwa amempiga chenga
golkipa wa Mgambo JKT, aliyedondoka huku akielekea kwenye goli la timu
hiyo wakati wa mchezo huo.
Mashabiki wa Simba wakifuatilia
mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya timu hiyo dhidi ya Mgambo JKT ya
Tanga, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam .
Hadi mwisho wa mchezo huo, Simba ilikuwa imeshinda mabao 4 na JKT Mgambo 0.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269