Mchezaji wa zamani wa timu ya
Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Kureshy Ufunguo (Kushoto) akioneshwa
mipira inayofaa kwa ajili ya kufundishia watoto kutoka kwa Mkurugenzi wa
Masoko wa Kampuni ya Isere Sports, Abbas Ally.
Mchezaji wa zamani wa Timu ya
Taifa ya Tanzania (Taifa Stars),Kureshy Ufunguo (Kulia) akipokea jezi
kwa ajili ya kuanzisha shule ya mafunzo ya watoto wadogo.
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya
Isere Sports, Abbas Ally (Kulia) akimkabidhi vifaa vya kuweka alama
uwanjani wakati wa mafunzo mchezaji wa zamani wa Simba na Taifa Stars,
Kureshy Ufunguo aliyeamua kuanzisha shule ya watoto.
Mchezaji wa zamani wa Simba na
Taifa Stars, Kureshy Ufunguo (Kulia) akiangalia kikombe kwa ajili ya
zawadi wa timu katika mashindano mbalimbali.
…………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
MCHEZAJI wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa
Stars), Simba, Kajumulo na Mirambo ya Tabora, Kureshy Ufunguo ameamua
kurudi uwanjani safari hii kuanzia Soka ya Watoto (Academy) ili kusaka
vipaji vya wachezaji wa kuunda Stars baadaye.
Mkurugenzi wa Masoko wa Isere Sports, Abbas Ally alisema
Kampuni yake itasaidia kutoa vifaa vya kuanzia mazoezi kama vikinga
ugoko (shin guard), mipira na jezi za mazoezi.
Alisema Kampuni itaendelea kutoa misaada kwa mchezaji huyo
kwani ni wachache wenye ndoto ya kufufua soka ya Tanzania ambayo kwa
sasa Stars haifanyi vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269