Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wakili Elias Nawera akizungumza na vijana wa Kata ya Kawe.
Kada
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Dar es Salaam, Wakili Elias
Nawera ambaye ametangaza nia ya kuwania Ubunge wa Jimbo la Kawe kupitia
CCM akizungumza na wananchi hasa vijana kwenye fainali ya mpira wa miguu
kati ya timu ya Halisi FC na Stand United zilizofanyika viwanja vya
Tanganyika Peackers Kawe Dar es Salaam jana ambapo aliwaomba ifikapo
Julai 4 mwaka huu kujitokeza kwa wingi kujiandika katika daftari la
kudumu la wapiga kura.
Mgombea
nafasi ya ubunge Iringa mjini, Ramadhan Yusuph 'Potipoti' ambaye
ametangaza nia akizungumza na wananchi wa Kawe katika fainali hizo.
Mgombea
nafasi ya ubunge Iringa mjini, Ramadhan Yusuph 'Potipoti' ambaye
ametangaza nia akizungumza na wananchi wa Kawe katika fainali hizo.
Watangania ya ubunge, Wakili Elias Nawera na Ramadhan Yusuph 'Potipoti' (kulia), wakiteta jambo katika fainali hizo.
Vijana wa Kawe wakiangalia fainali hiyo.
Mchezo ukiendelea. Stand Unated ilishinda mabao 5-4.
Mchezo ukiendelea.
Mashabiki wa timu ya Stand Unated wakiwazihaki wenzao wa Halisi FC baada ya kuwafunga kwa kubeba jeneza na msalaba wake.
Mashabiki wa timu ya Halisi FC wakishangia kwa kucheza baada ya timu yao kupata bao la pili.
Watoto wakifuatilia mashindano hayo.
Dotto Mwaibale
Dotto Mwaibale
TIMU
ya Stand United, imeibuka bingwa baada ya kuichapa Halisi FC kwa
changamoto ya mikwaju 5-4 katika fainali iliyofanyika kwenye viwanja vya
Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, Stand imezawadiwa jezi seti mbili na sh. 400,000 wakati mshindi wa pili alipata jezi seti moja na sh. 100,000.
Akizungumza
kabla ya kuanza kwa fainali hiyo, Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),
Mkoa wa Dar es Salaam, Wakili Elias Nawera ambaye ametangaza nia ya
kuwania Ubunge wa Jimbo la Kawe kupitia CCM aliwataka wananchi
kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kujiandikisha katika daftari la kudumu
la wapiga kura ambapo kwa Mkoa wa Dar es Salaam itakuwa ni Julai 4,
mwaka huu.
"Ndugu
zangu pamoja na mashindano haya ambayo yanatuunganisha na kutupa
burudani naomba Julai 4, mwaka huu kujitokeza kwa wingi kujiandikisha
bila kujali muda mfupi utakaokuwepo" alisema Nawera.
Akizungumzia
kuhusu watu wanaovamia maeneo ya wazi waliyotengwa kwa matumizi mengine
alisema watu wa kwanza kuchukua hatua ni wananchi wenyewe mahali alipo.
Katika fainali hizo, pia alihudhuria mgombea nafasi ya ubunge Iringa mjini, Ramadhan Yusuph 'Potipoti' ambaye ametangaza nia.
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269