Sheikh Sharifu Msopa akisisitiza jambo
wakati akizungumza na wanahabari Dar es Salaam leo Hoteli ya Shamoloon
iliyopo Sinza kuhusu maombi hayo maalumu.
Sheikh
Sharifu Msopa (kulia), akizungumza na wanahabari Dar es Salaam leo
Hoteli ya Shamoloon iliyopo Sinza kuhusu maombi hayo maalumu. Kshoto ni
Sheikh Maulana Salim.
Sheikh Maulana Salim (kushoto), akizungumza na wanahabari katika mkutano huo.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali na bloggers
wakichukua taarifa hiyo.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Na Dotto Mwaibale
SHEIKH Sharifu Msopa ametoa ofa kwa
viongozi na wananchi nchi nzima ya kuwafanyia maombi pamoja na kuwapaka
mafuta maalumu ya uponyaji kutoka Guba ya Uajemi.
Sharifu Msopa ametoa ofa hiyo wakati
akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, ambapo alisema
walengwa zaidi ni watu maskini, viongozi mbalimbali wale waliotangaza
nia ya kugombea nafasi mbalimbali kuelekea uchaguzi mkuu.
Alisema lengo la maombi hayo ambayo
hayachagui dini ni kuwapata viongozi waliochaguliwa na mungu ambao
wataliongoza taifa wakiwa na hofu ya mungu.
"Maombi tutakayofanya hayambagui mtu na
dini yake kwani tumekuwa tukitoa huduma hii ya maombi bure kwa
kushiriana na wenzetu wa kristo na tayari baadhi ya viongozi tumeanza
kuwafanyia maombi na yule aliyetayari awasiliane nasi" alisema Sharifu
Msopa.
Msopa alisema suala hilo la imani ni
muhimu sana hasa katika kipindi hichi cha kuelekea uchaguzi mkuu na kuwa
lengo kubwa ni kuona nchi inapata viongozi waliobora na si bora
viongozi kupitia maombi yao.
Alisema baada ya kufanyiwa maombi mtu
husika atapakwa mafuta ya ajabu kutoka Guba ya Uajemi ambayo yananguvu
ya kuondoa mikosi, uchawi na kumletea bahati muombewaji.
Alisema hivi sasa wapo katika maombi ya
mwezi mzima ya kuwaombea, viongozi wa siasa serikali, wafanyabiashara,
maskini na makundi mengine ili wapate neema hiyo.
Msopa alisema anaamini kuwa kupitia
maombi kiongozi mzuri atapatikana kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na
urais na kuwa mara baada ya mtu husika kupakwa mafuta hayo kama atakuwa
na uchawi, nuksi na mambo mengine yatamtoka kwa njia ya kuharisha,
kutapika na kumfanya awe huru.
Alisema maombi hayo anatarajia kuyafanya nchi nzima kwa kukutana na makundi ya watu mbalimbali wakiwemo wanafunzi.
Alisema kwamba maombi kama hayo amekuwa
akiyafanya katika nchi mbalimbali duniani na yamewasaidia watu wengi
kutoka dini zote za kikrito na waislamu na amekuwa akiyafanya bure. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269