Breaking News

Your Ad Spot

Oct 8, 2015

DK MAGUFULI AZISAMBARATISHA NGOME ZA MBOWE, NDESAMBURO NA NASSARI

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, John Magufuli akijinadi kwa wananchi katika mkutano wa kampeni kwenue Uwanja wa Mashujaa, mjini Moshi, Kilimanjaro. Ameivunja ngombe ya Chadema iliyokuwa inaoongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini, Philemon  Ndesamburo

Dk Magufuli ambaye hadi sasa amefanya kampeni katika mikoa 22 kwa kusafiri kwa barabara kwa tkribani Km 20,000, amesema kuwa yeye ni rais kwani  anasubiri tu kuapishwa, baada ya uchaguzi. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
 Wakazi wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro wakisikiliza kwa makini wakati Dk Magufuli akiwahutubia na kuwaomba kura mjini Bomang'ombe, Jimbo la Hai lililokuwa linaonggozwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
 Dk Magufuli akiwahutubia wananchi katika mkutano wa kampeni katika Mji wa Bomang'ombe, wilayani Hai leo.
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akimtambulisha Katibu wa Chadema Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Jubilant Lema ambaye alitangaza kukihama chama hicho na kujiunga na CCM wakati wa mkutano wa kampeni mjini Bomang'ombe
 Akina dada wakishangilia kwa furaha baada ya kumona Dk Magufuli akiwasili kwenye mkutano wa kampeni eneo la Usa River Jimbo la Arumeru Mashariki.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk Magufuli akisalimiana na  Mkuu wa Majeshi mstaafu, Jenerali mstaafuMirisho Sarakikyawa mkutano wa kampeni mjini Usa River, Jimbo la Arumeru Mashariki, mkoani Arusha.
 Dk Magufuli akijinadi katika mkutano wa kampeni katika Mji wa Usa River, Arusha leo.
 Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Arumeru Mashariki John Pallangyo wakati wa mkutano wa kampeni katika Mji wa Usa River, Arusha.
 Wagombea udiwani kupitia CCM Jimbo la Arumeru Mashariki wakijitambulisha kwa wananchi wakati wa mkutano huo wa kampeni katika Mji wa Usa River
 Wananchi wakinyoosha mikono ikiwa ni ishara ya kukubali kumpigia kura ZA URAIS  Dk Magufuli Oktoba 25, MWAKA HUU.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Dk Magufuli akisalimiana na Emmanuel Nchimbi wakati wa kampeni za  CCM wilayani Siha leo.
 Sehemu ya wananchi katika mkutano wa kampeni mjini Siha, Mkoa ni Kilimanjaro
 Dk Magufuli akijinadi kwa wananchi katika Jimbo la Siha, mkoani Kilimanjaro leo
 Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Siha,AggreyMwanry wa mkutano wa kampeni
 Moja ya mabango yaliyokuwepo kwenye mkutano wa kampeni katika mkutano uliohutubiwa na Dk Magufuli katika Jimbo la Hai
 Dk Magufuli akimnadi mgombea ubunge Jimbo la Hai kupitia CCM, Dastan Millya wa mkutano wa kampeni mjini Bomang'ombe, Jimbo la Hai, Kilimanjaro.
 Mma aliyejulikana kwa jina la Rukia, akivalishwa kofia na Dk Magufuli baada ya kutangaza kujiunga na CCM kutoka Chadema.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Wakazi wa Uru, Jimbo la Moshi Vijijini, wakishangilia baada ya kufurahishwa na hotuba za Dk Magufuli katika mkutano wa kampeni
 Dk Magufuli akimkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya CCM, Mgombea ubunge Jimbo la Moshi Vijijini, Cyril Chami Ilani ya Uchaguzi ya CCM, wakati wa mkutano wa kampeni Uru, Kilimanjaro
 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Ushirika Moshi, wakishangilia baada ya kuahidiwa na Dk Magufuli kuwa atasimamia suala la mikopo kwa wanafunzi ili wawe wanapata kwa muda muafaka.
 Dk Magufuli akimpongeza aliyewahi kuwa mgombea ubunge Jimbo la Monduli 2010,Ole Silanga livyomsabaratisha Mgombea urais kupitia Chedema, ambapo alidai ni Dikteta anayewatesa wananchi wa Jimbo la Monduli alipokuwa Mbunge wa Jimbo hilo na Waziri Mkuu.
 Wimbo uliotungwa na wasanii wa Tanzania unaosisitiza kutunza amani iliyopo wakiimba wakati wa mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Moshi, Kilimanjaro
 Mgombea ubunge Jimbo la Simanjiro, Christopher Ole Sendeka akimuombea kura Dk Magufuli na kuwashawishi watanzania kutompigia kura Mgombea wa Ukawa, Edward
 Emmanuel nchimbi akimuombea kura Dk Magufuli katika mkutano huo
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Abdallah Bulembo, akielezea wasifu wa Dk Magufuli na kuwaomba wananchi kumpigia kura
 Sehemu ya wananchi wakiwa katika mkutano wa kampeni za CCM kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Moshi
 Dk Magufuli akiwaimbisha wananchi wimbo wa Aliselema Aleja wakati wa mkutano huo wa kampeni kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Moshi
 Viongozi wa CCM, Kutoka kushoto
 Dk Magufuli akimnadi kwa wananchi mgombea ubunge Jimbo la Moshi Mjini, Davis Mosha wakati wa mkutrano wa kampeni kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Moshi.
 Dk Magufuli akimvisha kofia mmoja wa wanachama wa Chadema aliyehamia CCM wakati wa mkutano wa kampeni mjini Moshi
 Dk Magufuli akiwahesabia baadhi ya viongozi waliokuwa wakifanya mazoezi ya Push Up mjini Moshi. Wa tatu kulia ni Mgombea ubunge Jimbo la Moshi Mjini, Davis Mosha.
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya  Juma Nature, akitumbuiza wakati wa mkutano huo.Kushoto ni mchekeshaji Ally Yanga.
 Baadhi ya wananfunzi wakishiriki kuimba wimbo wa wasanii wa kudumisha amani iliyopo
 Dk Magufuli akisalimiana na msanii Juma Nature
 Msanii Fid Q akitumbuiza wakati wa mkutano huo
Wananchi wakishangilia baada ya kufurahishwa na ahadi mbalimbali zilizokuwa zinatolewa na Dk Magufuli, ikiwemo ya Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha nne.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages