Breaking News

Your Ad Spot

Oct 8, 2015

RAIS JAKAYA KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI LA JENGO LA MOROCCO SQUARE JIJINI DAR ES SALAAM

 
 Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akifungua pazia kuashiria  uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa Jengo la Morocco Square Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la  Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.
 Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akisalimiana na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa Jengo la Morocco Square.
 Rais Jakaya Kikwete (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa  (NHC), Zakhia Meghji (kulia) na Waziri wa Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi, William Lukuvi wakipiga makofi kumpongeza Rais Kikwete katika siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika sanjari na hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la jengo hilo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa  (NHC), Zakhia Meghji (wa pili kulia), akimkabidhi zawadi ya sherehe yake ya kuzaliwa.

 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakifungua shampeni kumpongeza Rais Kikwete katika siku yake hiyo ya kuzaliwa.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la  Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia), wakati wa hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la jengo hilo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la  Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akiteta jambo na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki wakati wa hafla hiyo.
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Waandishi wa habari wakiwa kwenye hafla hiyo.
 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakiwa kwenye sherehe hiyo.
 Wadau mbalimbali na Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Rais Jakaya Kikkwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi 
wa NHC.

Na Dotto Mwaibale

RAIS Jakaya Kikwete amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa, (NHC), chini ya Mkurugenzi wake Nehemia Mchechu kwa mradi wa ujenzi wa jengo la Moroco Square ambao utagharimu sh.bilioni 150 za kitanzania hadi kukamilika kwake.

Mradi wa ujenzi huo utakamilika mwaka 2017 na jengo litakuwa na mita za mraba 110,000 na ukiwa na majengo manne.Mawili ni kwa ajili ya ofisi , moja hoteli na nyingine nyumba za makazi ya watu 100, ghorofa 20 na kiwanha cha  ambapo mawili ni kwa ajili ya ofisi, moja Hoteli na lingine ni kwa ajili ya nyumba za makazi ya watu 100 , ghorofa 20 lenye eneo la kiwanja cha ndege kwa juu yake.

Akizungumza Dar es salaam jana, wakati wa uwekaji jiwe la msingi wa ujenzi wa eneo hilo jana, Rais Kikwete alisema mradi huo ni mkubwa kuliko yote katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na utaifikisha nchi katika hatua nyingine za kimaendeleo.

Aliongeza kuwa ni mambo mapya kuanzishwa Tanzania tofauti na siku za nyuma, hivyo alilipongeza NHC kwa kwenda na wakati. 

Rais Kikwete alisema utakapokamilika mradi wa eneo hilo la Mororco Square utakuwa na faida nyingi kama kupunguza gharama za wananchi kwenda mijini kutokana na huduma zote za kijamii kupatikana eneo hilo.

Alitoa mwito kwa NHC kufungua huduma ya Online ili watu wasipate shida wawe wanafanya kila kitu kupitia mitandao badala ya kuhangaika barabara kwenda kutafuta huduma na matokeo yake wanapoteza muda.

Alisema katika kuhakikisha huduma zinafanyika kwa urahisi inabidi ziwekwe barabara za juu ili watu wanaopita katika eneo hilo wavuke salama.

"Pale Morocco kuna njia nne, hivyo kinachotakiwa ni kuweka barabara ya juu lakini sijui kama itawezekana kutokana na kuwa namaliza muda wangu, lakini nawaahidi kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za NHC, hivyo changamoto zenu zitatatuliwa "alisema.

Kwa upande wake, Mchechu alifafanua eneo hilo litakuwa na viwanja vya michezo kwa watoto, maduka hivyo ni kitovu cha kuchangamsha mji kutokana na kuwa lipo katikati ya mji. 

Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Zakhia Meghji alisema anaamini kuwa Rais ajaye ni Dk.John Magufuli, hivyo anaamini ataendeleza mradi huo aliouacha Kikwete.

Alisema umefika wakati wa kutungwa sheria itakayowezesha wageni kununua nyumba hizo kutokana na iliyopo hairuhusu ili kupanua soko kwa wateja.

Mradi huo umefanikiwa kwa kupata mkopo wa fedha kutoka Benki ya CRDB chini ya uongozi wa Mkurugenzi Mkuu, Dk. Charles Kimei.


No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages