Maafisa wa polisi wa trafiki
wametumwa ili kujaribu kumaliza msongamano wa magari ambao umechukua
siku mbili katika barabara kuu ya Mombasa Nairobi.
Barabara hiyo ni muhimu kwa uchumi wa jimbo hilo kwa kuwa inaunganisha bandari ya Mombasa na mataifa yasiokuwa na Bandari.
Eneo lililoathiriwa pakubwa ni lile la Taru,yapata kilomita 80 kutoka Mombasa.
Waandishi wanasema kuwa msongamano huo umesababishwa na marekebisho
yanayofanywa katika barabara kutokana na mvua kubwa inayoendelea
kunyesha.
Milolongo mirefu ya magari huwa jambo la kawaida nchini Kenya na haswa husababishwa na barabara mbovu ambazo hazirekebishwi.
Mabasi
ya abiria na malori yanayobeba mizigo na kupeleka Nairobi na kwengineko
ni miongoni mwa magari yaliokwama tangu mlolongo huo uanze siku ya
jumanne jioni.
Mmoja wa wasafari aliyehojiwa na runinga ya NTV amesema kuwa baadhi yao walikuwa wamekwama katika mlolongo huo kwa saa 48.
''Sijakula lolote.Nimeambiwa kwamba kuna magari mengi ambayo yamekwama katika trafiki''.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269