Balozi
wa Jumuiya ya Ulaya (EU), nchini Tanzania, Filiberto Ceriani Sebregondi
akifafanua jambo wakati wa hafla ya kutiliana saini mkataba wa
kuyapatia Mashirika ya Umoja wa Mataifa Euro 200,000. Hafla hiyo
ilifanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Uhusiano wa EU, Eric
Beaume. (Picha na Francis Dande)
Balozi
wa Jumuiya ya Ulaya (EU), nchini Tanzania, Filiberto Ceriani
Sebregondi (kulia) akibadilishana hati na Mratibu wa Mashirika ya Umoja
wa Mataifa, Alvaro Rodriguez wakati wa hafla ya kutiliana saini mkataba
wa kuyapatia Mashirika ya Umoja wa Mataifa Euro 200,000. Hafla hiyo
ilifanyika jijini Dar es Salaam.
Balozi
wa Jumuiya ya Ulaya (EU), nchini Tanzania, Filiberto Ceriani
Sebregondi (kulia) akisaini hati na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa
Mataifa, Alvaro Rodriguez wakati wa hafla ya kutiliana saini mkataba wa
kuyapatia Mashirika ya Umoja wa Mataifa Euro 200,000.
Baadhi ya wageni waliohudhuria hafla hiyo. Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez akizungumza katika hafla ya kutiliana saini mkataba wa kuyapatia Mashirika ya Umoja wa Mataifa Euro 200,000.
Baadhi ya wageni waliohudhuria hafla hiyo. Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez akizungumza katika hafla ya kutiliana saini mkataba wa kuyapatia Mashirika ya Umoja wa Mataifa Euro 200,000.
Na Mwandishi Wetu
JUMUIYA
ya Ulaya (EU)imetiliana saini na Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo
nchini yanayofanya kazi kama shirika moja (One UN), ruzuku Euro 200,000
sawa na sh. Milioni 478.
Utilianaji saini huo ulifanywa na Mratibu wa Mashirika ya UN nchini , Alvaro Rodriguez na Balozi wa EU, Filiberto Sebregondi.
Sebregondi
alisema Tanzania imefanikiwa kutengeneza mfano wa namna bora Mashirika
ya UN yanavyoweza kufanyakazi kama taasisi moja katika kuboresha maisha
ya watu.
Naye
Rodriguez, alisema fedha hizo zimelenga kusaidia miradi ya pamoja ya EU
NA UN ya mawasiliano, uragibishi, uimarishaji wa ufuatiliaji na uwazi.
Rodriguez,
alisema msaada huo ni muhimu katika ufanisi wa maendeleo kwa Tanzania
wakati nchi inajipanga kutekeleza malengo ya endelevu SDGs.
“Nchi
ina Rais mpya na inahitaji kuwa ya kipato cha kati sisi UN na washirika
wetu ni vyema tukaunga jitihada hizi ili kusiwepo na mtanzania
atakayeachwa nyuma katika mchakato wa maendeleo,” alisema.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269