Kaimu Mkurugenzi Mtendaji mpya
wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru
akifafanua jambo katika mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa hospitali
hiyo leo. Kushoto ni Katibu wa Baraza hilo, Clive Leonard Urima na kulia
ni Katibu msaidizi, Domiana John.
Mwakilishi wa Chama cha
Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE), Fortunatus Chuwa akichangia
mada kwenye mkutano wa Baraza la Wafanyakazi ambao umefanyika leo
jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa wafanyakazi wa
hospitali hiyo, Cresensia Joseph John akichangia mada kwenye mkutano wa
Baraza la Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
Katibu wa Chama Cha
Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE), Gaudensi Kadyango
akiwasilisha mada kwenye mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Hospitali
ya Taifa ya Muhimbili (MNH). Mkutano huo umefanyika leo jijini Dar es
Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali
ya Taifa ya Muhimbili (MNH) wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
hospitali hiyo, Profesa Lawrence Mseru kwenye mkutano wa Baraza la
Wafanyakazi.
PICHA ZOTE KWA HISANI YA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI (MNH)
…………………………………………………………………….
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru leo
amekutana na Baraza la Wafanyakazi la Hospitali hii katika kikao cha 15
cha Baraza hili.
Katika kikao hicho wafanyakazi
wamezungumzia changamoto zinazoikabili MNH na mafaniko mbalimbali
yaliopatikana yakiwamo uboreshaji wa miundo mbinu na upatikanaji wa
huduma kwa kiwango cha juu.
Profesa Museru amewataka
Wakurugenzi, Wakuu wa Idara pamoja na Mameneja wa Majengo kusimamia
vizuri wafanyakazi wa MNH watimize wajibu wao ili kuongeza tija mahali
pa kazi.
“Kila mmoja anapaswa kutekeleza
majukumu yake kwa mujibu wa sheria na mkataba wake wa kazi ili kufikia
malengo,”amesema Kaimu Mkurugenzi Mtendaji huyo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269