Breaking News

Your Ad Spot

Nov 12, 2015

KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI , VIJANA, UTAMADUNI, NA MICHEZO AFANYA ZIARA BASATA, TBC NA TSN.

01
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel (wa kwanza kushoto) akiangalia mitambo ya kurushia matangazo ya Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) wakati alipofanya ziara ya kikazi katika minara ya shirika hilo leo hii Kisarawe.Profesa Elisante amefanya ziara katika Taasisi tatu zilizo chini ya Wizara hiyo ambazo ni Baraza la Sanaa Tanzabia (BASATA),Tanzania Standard Newspapers (TSN) na Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) lengo likiwa ni kufahamiana na wafanyakazi,kuwahimiza kufanya kazi kwa bidii na kujua changamoto zinazowakabili ikiwa ni kutimiza kauli mbiu ya HAPA KAZI TU ya awamu ya Tano.Anaefuatia ni mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Bw.Clement Mshana.
02
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akiangalia tofauti ya santuri ya zamani na flashi ya kisasa zinavyozidiana ukubwa kwa umbo alipotembelea maktaba mojawapo katika ofisi za shirika la utangazaji Tanzania (TBC) alipofanya ziara kuongea na menejimenti ya shirika ilo leo jijini Dar es Salaam.Santuri zilitumika kipinda shirika hilo likiitwa Radio Tanzania Dar es Salaam.(RTD).
03
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel(waliosimama watatu kulia) akiwa katika mojawapo ya studio za kurushia matangazo ya shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wwakati alipotembelea shirika ilo leo kuongea na menejimenti yake pamoja na kuona utendaji wake.
04
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel(aliyekaa mwenye miwani) akipata maelekezo jinsi gazeti linavyotengenezwa kutoka kwa mtumishi wa Standard News Papers(TSN) leo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kikazi na kuangalia utendaji wa kazi.
05
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel (wa pili kulia) akiangalia moja ya kazi za vijana wanojifunza kutengeneza batiki na kuweka chapa alipotembelea ofisi za Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA) leo hii jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages