Breaking News

Your Ad Spot

Feb 19, 2016


NA K-VIS MEDIA/Na Mashirika ya Habari
KINANARA wa upinzani nchini Uganda, Kanali Dkt. Kizza Besigye amekamatwa na polisi leo Ijumaa Februari 19, 2016, huku Rais wa sasa Yoweri Kaguta Museveni akiongoza kwenye matokeo ya awali ya kura ambazo zimehesabiwa hadi sasa.
Polisi wa kutuliza ghasia walifyatua mabomu ya kutoa machozi jijini Kampala, eneo ambalo kiongozi huyo wa upinzania kutoka chama cha Forum for Democratic Change, (FDC), ana wafuasi wengi. Uchaguzi Mkuu wa Nchi hiyo ulifanyika Alhamisi Februari 18, 2016 na umeelezwa kuwa ulikuwa mtulivu na wa amani licha ya kasoro chache zilizojitokeza kwenye baadhi ya maeneo ambapo vifaa vya kupigia kura vilichelewa kufika.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Nchini Uganda, Injinia Badru Kigundu, amewaambia waandishi wa habari kuwa kwa wale waliofanya fujo na kuharibu vifaa vya kupigia kura, wasitegemee uchaguzi kufanyika kwenye eneo hilo na badala yake wasubiri uchaguzi mwingine mwaka 2021.
Hii ni mara ya pili chini ya masaa 245 Dkt. Besigye anakamatwa na polisi. Alhamisi jioni majira ya saa 12, Dkt. Besigye alizuiwa na polisi, ambapo walisema wanamzuia kwa usalama wake ili asidhuriwe na wafuasi wake, ingawa baadaye walimuachia.
Dkt. Besigye ambaye alikuwa mshirika wa karibu wa Rais Museveni kabla ya kuhitilafiana, amedai uchaguzi huu sio huru na wa haki na kusema kuwa “Madikteta Duniani kuondolewa kwa mapinduzi kama sio kifo.”.
Matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa Jumamosi Februari 20, 2015

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages