Breaking News

Your Ad Spot

Feb 17, 2016

KAMBI YA BOKO HARAM YAHARIBIWA NIGERIA


Jeshi la Nigeria limesema kuwa limeharibu kambi za wapiganaji wa Boko Haram katika vijiji vya Doro na Kuda kaskazini mashariki mwa jimbo la Borno.
Wapiganaji wanne wa kundi hilo waliuawa huku wengine wawili wakikamatwa wakati wa oparesheni katika misitu ya eneo la Alagarno na Sambisa,kulingana na msemaji wa jeshi kanali sani Usman.
Wanajeshi watatu na raia wanne walijeruhiwa katika mapigano hayo, alisema.
Pikipiki,farasi na Punda walipatikana katika kambi hiyo.
Kundi la Boko haram limepoteza eneo kubwa lililokuwa likidhibiti, lakini bado linatekeleza milipuko mibaya ya kujitolea muhanga.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages