Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu (kulia), akimpongeza Katibu Mkuu wa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira, mara baada
ya Katibu Mkuu huyo kumaliza kutoa hotuba ya kufunga Mkutano wa Mwaka wa
Maafisa Waandamizi wa Jeshi hilo uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa
Mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira (kulia),
akipokelewa na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Ilala, SACP Lucas Mkondya, alipofika
kufunga kikao kazi cha Maafisa
Waandamizi wa Jeshi la Polisi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu
Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira,
akizungumza wakati wa kufunga kikao kazi
cha Maafisa Maandamizi wa Jeshi la Polisi katika Ukumbi wa Mikutano wa
Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. Wapili kulia meza
kuu ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu.
Mkuu
wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu, akizungumza na Maafisa Waandamizi wa
Jeshi la Polisi nchini wakati wa kufungwa Mkutano wa Mwaka wa Maafisa hao
uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es
Salaam.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira
(wanne kushoto waliokaa), Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu (kushoto
kwa Katibu Mkuu) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa Waandamizi wa Jeshi
la Polisi, mara baada ya kufungwa Mkutano wao wa Mwaka uliofanyika katika Ukumbi
wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. (Picha
zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269