Breaking News

Your Ad Spot

Feb 21, 2016

MOROCCO YAZIMA SHAMBULIO LA DAESH, MAGAIDI KADHAA

Morocco yazima shambulio la Daesh, magaidi kadhaa wakamatwa
Morocco imesema kuwa imefanikiwa kuzima shambulio la kemikali lililokuwa limepangwa kufanywa na mtandao mmoja wa kigaidi unaohusishwa na kundi la kitakfiri la Daesh.
Abdelhak Khiame, Mkurugenzi wa Idara ya Upelelezi nchini humo, leo Jumapili amesema kuwa, vyombo vya usalama vya nchi hiyo vimekamata makopo yaliyokuwa na kemikali ya sumu aina ya salfa, wakati wa operesheni yao kwenye ngome za magaidi hao katika miji mbalimbali.
Amesema, magaidi hao wanaoaminika kuwa na mafungamano na Daesh hawakupokea mafunzo kutoka kambi za kundi hilo nchini Iraq ama Syria, lakini wamekuwa wakipokea mafunzo na ufadhili kutoka kwa Daesh kupitia njia zisizo za moja kwa moja. Mkurugenzi wa Idara ya Upelelezi wa Morocco amesema silaha walizozikamata wakati wa operesheni hiyo zinatoka Libya. Miongoni mwa watuhumiwa waliokamatwa katika msako huo ni kijana mmoja wa miaka 16 ambaye alikuwa amefundishwa namna ya kuripua magari kwa bomu.
Kwa mujibu wa takwimu rasmi za Morocco, raia zaidi ya 1,300 wa nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika wamejiunga na Daesh kufikia sasa na kwamba 246 kati yao wamekwishauawa nchini Syria na wengine 40 nchini Iraq. Imearifiwa kuwa 156 kati ya magaidi hao ambao walikuwa wameenda Syria na Iraq, wamefanikiwa kurejea nchini humo kwa lengo la kufanya mashambulio mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages