Polisi katika mji
mkuu wa Somalia Mogadishu wanasema kuwa wanamgambo wa al-Shabab wamewaua
takriban watu 9 wakati wa shambulizi kwenye hoteli moja iliyo karibu na
ikulu ya rais.
Ripoti zinasema kwa mshambuliaji wa kujitolea
muhanga aliendesha gari katika lango la hoteli hiyo kabla ya watu
waliokuwa na silaha kuingia ambapo ufyatulianaji wa risasi ulianza na
walinzi wa hoteli.
Kundi la wanamgambo la Al Shabaab linesema kuwa liliendesha shambulizi hilo
Al
Shabab walikuwa wikidhibiti sehemu nyingi za mji wa Mogadishu kabla ya
kuondoka lakini wanaendesha mashambulizi ya mara kwa mara.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269