Bibi. Florence Mwanri, Naibu Katibu Mtendaji, Tume ya
Mipango, alipata pia fursa ya kutembelea kiwanda cha TEMSO Engineering
kinachozalisha vifaa mbalimbali vya ujenzi kama vile mashine za kufyatulia
matofali na matoroli (wheelbarrows).
Viongozi na maofisa kutoka Tume ya Mipango wakipata
maelezo kutoka kwa Bw. Abdallah Kayumbi (wa kwanza kulia) kuhusu uzalishaji wa
vifaa vinavyotumika kuzalisha nishati ya umeme kwa kutumia upepo (wind
Turbines).
Omar Jumanne Bakari (wa tatu kulia) Mkurugenzi Mkuu wa Shirika
la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO) akitoa maelezo kwa timu ya wataalam
kutoka Tume ya Mipango ikiongozwa na Bibi. Florence Mwanri Kaimu Katibu
Mtendaji wa Tume ya Mipango kuhusu ufanisi wa mashine ya kutengenezea sabuni
katika kiwanda kidogo cha sabuni ambazo soko lake linapatikana jijini Dar es
Saalam na mikoa ya jirani.
Viongozi na maofisa kutoka Tume ya Mipango na SIDO
wakiangalia mashine ya kuzalisha nyuzi kwa ajili ya kutengeneza nguo
inavyofanya kazi katika kiwanda cha Fruitful Goshen, Matengenezo Textile.
Omar Jumanne Bakari, Mkurugenzi Mkuu wa SIDO (aliyesimama), akitoa maelezo kwa
viongozi na maofisa kutoka Tume ya Mipango (waliokaa kushoto) kuhusu SIDO
inavyofanya kazi katika kuwasaidia wazawa ili kukuza uwekezaji katika viwanda
vidogo vidogo. Waliokaa kulia ni wamiliki wa viwanda vidogovidogo wanaofanya
shughuli zao chini ya SIDO.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269