Utafiti mpya unaonyesha kuwa mwanya kati ya matajiri na masikini unazidi kupanuka nchini Marekani.
Gazeti la Wall-Street Journal limechapisha ripoti inayoonyesha
kuwa mlingano wa kijamii unazidi kutokomea miongoni mwa Wamarekani
ambapo Masikini wanazidi kulemewa na uchochole nao matajiri wanazidi
kujilimbikizia mali kila uchao. Utafiti huo mpya umefichua kuwa, jamii
ya Wamarekani weusi imezidi kutengwa na kunyimwa nafasi sawa na wenzao
weupe jambo linalozidi kupanua pengo kati ya matajiri na masikini.
Utafiti huo umetumia vigezo vya afya, ajira na umri wa kuishi watu ili
kuandaa ripoti hiyo mpya. Kwa mujibu wa watafiti ni kwamba Marekani
inaongoza kwa kuwa na ukosefu wa usawa katika jamii.
Ripoti hiyo imewanyooshea kidole cha lawama wanasiasa wa Marekani
ambapo wanatuhumiwa kuharibu mazingira ya uwekezaji na hivyo kuongeza
kiwango cha ukosefu wa ajira. Matokeo yake ni kupanuka mwanya kati ya
watu masikini na wale matajiri katika nchi hiyo inayohesabiwa kuwa na
uchumi mkubwa zaidi duniani.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269