Breaking News

Your Ad Spot

Mar 21, 2016

KILELE CHA MAADHIMISHO YA AFYA YA KINYWA NA MENO DUNIANI YAFANA MKOANI MOROGORO 2016

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya akifungua rasmi Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Afya ya Kinywa na Meno Kitaifa Mkoani Morogoro Machi 20, 2016. akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Steven Kebwe , katika viwanja vya Shule ya Msingi K.Ndege, zaidi ya wananchi  mia sita wamepatiwa Ushauri na tiba ya Afya ya kinywa na meno, kushoto ni Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro waHaspitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Aalaam na kulia ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno katika Hospitali hiyo Dk. Samson Tarimo .(PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro ( kushoto) akisalimiana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya kulia mara alipo wasili  viwanja vya Shule ya Msingi K.Ndege katika Maaadhimisho ya Kilele cha Wiki ya Afya ya Kinywa na Meno ambapo alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mkoa huo Steven Kebwe
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya kushoto akiwapungia wananchi mkono mara alipowasili katika Maadhimisho hayo, kulia ni Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro
Mc, ambaye ni Afisa Afya wa Mkoa wa Morogoro Carle Lyimo akisherehesha katika Maadhimisho hayo
Mwananchi  akiomba ufafanuzi wa Afya ya Kinywa na Meno wakati wa Maadhimisho hayo
Baadhi ya wajumbe, Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno wakiwa wanawasili katika Maadhimisho hayo Mkoani Morogoro akiwemo Profesa. Lembariti, kulia
Profesa Lembariti akitoa utambulisho
Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro (wa tatu kushoto) akiteta jambo na Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno, wote kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili Dar es Salaam, wakiwa katika  Kilele cha Maadhimisho ya Afya ya Kinywa na Meno Kitaifa Mkoani Morogoro, kulia ni Makamu wa Rais wa Chama hicho Dk. Ambege Mwakatobe,  kushoto ni Katibu wa TDA Dk. Tumaini Simon na Mwekahazina wa chama hicho   Dk.  Arnold  Mtenga




Baadhi ya Wananchi waliojitokeza kwenye Maadhimisho hayo

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya  (wa pili kushoto) akimzawadia Flana  mtoto  Sezali  Frank (13) baada ya kujibu maswali aliyoulizwa na mc jinsi ya upigaji mswaki na utunzaji wa mswaki kwa ujumla


Meya wa Manispaa ya Morogoro, Pascal Kihanga  akizungumza katika Maadhimisho hayo,
Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno katika Hospitali hiyo ya Mkoa,  Dk. Samson Tarimo wapili kulia alipokua akitambulisha Meza kuu
Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Theresia Mahongo  akizungumza katika Maadhimisho hayo
Meza kuu wakishiriki kuimba wimbo wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno pamoja na wananchi (hawapo pichani) waliofika katika Maadhimisho hayo









Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na Katibu Msaidizi wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno (TDA) Dk. Elizabeth Lyimo akijitambulisha wakati wa Maadhimisho hayo
  Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dr, Gustav Rwekaza akijitambulisha katika Maadhimisho ya Kinywa na Meno wakati wa Kilele cha Maadhimisho hayo Kitaifa Mkoani Morogoro Machi 20, 2016
Profesa Lembariti akijitambulisha


Profesa Lembariti akizungumza jambo na kutoa neno la shukrani kwa Mgeni Rasmi, wananchi pamoja na Madaktari wote walio jitokeza kusaidia na kutoa ahadi wapo pamoja na madaktari kwa muda wowote mara watapoomba msaada


Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya akijisajili katika daftari ili  kupata namba ya kwenda muona Dokta
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya akipata maelezo kutoka kwa Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Mazimbu Kampasi ya (Sua) Dk. Patrick Mwamwongi kulia


Mkuu wa Kitengo cha Afya ya Kinywa na Meno Hospitali ya Mkoa wa Morogoro na Mwenyekiti wa Maandalizi ya Kilele cha Maadhimisho ya  Afya ya Kinywa na Meno Dk. Baraka Nzobo (aliye vaa kofia) akimfanyia uchunguzi wa Kinywa, Mwanafunzi wa Darasa la Pili wa Shule ya Msingi Fransalian , Mashindike Matunge  (7)  wakati wa Kilele cha Maadhimisho hayo Mkoani Morogoro, kushoto ni Mama mzazi wa mwanafunzi huyo ambaye ni -Mtangazaji wa Planet Radio 87. 9 FM,  iliyopo Mkoani Morogoro, Doreen Mwinyi  mara alipofika na mwanaye huyo katika Kilele cha Maadhimisho ya Afya na Kinywa na Meno

Mwalimu wa Shule ya Msingi Uhuru ya Mkoani Morogoro Lidya Maira akiomba ufafanuzi kwa Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno,kuhusiana na kinywa.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya (watatu kulia) waliyo kaa,  akiwa katika picha ya pamoja ya viongozi wa mkoa wa Hospitali hiyo na madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Taifa Muhimbili
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya (wa pili kushoto) akiwaanaondoka kwenye maadhimisho hayo, wa kwanza kushoto ni Meya wa Manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga na kulia ni Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro
Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Theresia Mahongo kushoto akiagana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya alipokua akiondoa eneop la tukio
Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro akiagana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Wariambora Nkya
Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hospitali ya Mafinga Health Center ya Mkoani Morogoro Henael Kanyawana  akimpatia maelezo Mtangazaji wa Planet Radio 87. 9 FM,  iliyopo Mkoani Morogoro, Doreen Mwinyi  mara alipofika katika Kilele cha Maadhimisho ya Afya na Kinywa na Meno
Catherine Gemba wa Kituo cha Afya Kingolwira Manispaa ya  Morogo akiwaandikisha katika Daftari na kuwapatia namba wananchi hao na kwenda muona Daktari wakati wa Maadhimisho hayo
Daktari wa Afya ya Kinywa na Meno wa Hosptali ya Taifa Muhimbili Dk. Germana Vincent kulia akimfanyia mwananchi ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja ambaye alifika katika Maadhimisho hayo kupata huduma hiyo ya Kinywa

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages