Breaking News

Your Ad Spot

Jul 8, 2016

WENGI WAJIUNGA NA MFUMO WA ‘WOTE SCHEME’ WA MFUKO WA PENSHENI WA PPF KATIKA MAONESHO YA SABASABA

 Maafisa wa Mfuko wa PPF, wakitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda hilo kuhusu Mfumo wa ‘Wote Scheme’ katika maonesho ya 40 ya Biashara ya KImataifa kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Picha na Mafoto Blog
 Maafisa wa Mfuko wa PPF, wakitoa elimu kwa wananchi waliotembelea Banda hilo kuhusu Mfumo wa ‘Wote Scheme’ katika maonesho ya 40 ya Biashara ya KImataifa kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Afisa Michango wa Mfuko wa PPF, Glory Maboya, akizungumza na mteja aliyefika katika Banda hilo kujua michango yake katika Maonesho ya Sabasaba.
 Baadhi ya Wananchi wakipata huduma kutoka kwa Maafisa wa PPF katika Banda la Maonesho kwenye Viwanja vya Sabasaba.
Mmoja wa wanachama waliojiunga na Mfuko huo akijaza fomu.
 Balozi wa Tanzania Nchini Saudi Arabia, Mhe. Hemedi Iddi Mgaza (kulia) akimkabidhi Kitambulisho Azda Amani, Mwanachama wa Mfuko huo kupitia Mfumo wa Lazima, aliyejiunga pia na Mfumo mpya wa ‘Wote Scheme’ katika Maonesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere.
 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF, Dkt. Aggrey Mlimuka (kulia) akimkabidhi Kitambulisho Mwanachama mpya, Eliuter Ernest, aliyejiunga na Mfumo wa ‘WoteScheme’ baada ya kupata elimu kutoka kwa maafisa wa Mfuko huo.
 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF, Dkt. Aggrey Mlimuka (kulia) akimkabidhi Kitambulisho Mwanachama mpya, Brasis Mkude, aliyejiunga na Mfumo wa ‘WoteScheme’ baada ya kupata elimu kutoka kwa maafisa wa Mfuko huo.
 Balozi wa Tanzania Nchini Saudi Arabia, Mhe. Hemedi Iddi Mgaza (wa Nne kutoka kulia) Meneja wa PPF Kanda ya Kinondoni, Zahra Kayugwa (wa tano kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wafanyakazi wa PPF waliopo katika Banda la Maonesho la Mfuko huo kwenye Maonesho hayo.
 Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni wa PPF, Dkt. Aggrey Mlimuka (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Mfuko huo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages