Mgombea urais wa chama cha
Democratic Hillary Clinton ameelezea masikitiko yake alipojitokeza
hadharani mara ya kwanza tangu ashindwe kwenye uchaguzi wa rais nchini
Marekani na Donald Trump wa chama cha Republican.
Bi Clinton, akihutubu mjini Washington DC amesema alikuwa hataki kutoka nyumbani tena.
Ameambia shirika la kuwasaidia watoto wasiojiweza kwamba uchaguzi huo umewafanya Wamarekani wengi kutafakari.
- Hillary Clinton aenda kutembea porini
- Hillary: Trump apewe fursa ya kuongoza
- Kwa Picha: Maisha ya Clinton na Trump
Bi Clinton aliongoza kwa wingi wa kura za kawaida lakini
akashindwa kinyang'anyiro cha urais kupitia kura za wajumbe, ambazo
ndizo huamua mshidni wa urais.
"Sasa, nitakiri kwamba kuja kwangu
hapa halikuwa jambo rahisi," alisema alipokuwa akitunukiwa heshima na
wakfu wa Children's Defense Fund.
"Kuna nyakati kadha wiki hiyo
moja iliyopita ambapo nilitaka kujikunyata tu nikiwa na kitabu kizuri na
nisiwahi kutoka nje ya nyumba tena."
Aliendelea: "Ninajua wengi wengu mmevunjwa moyo sana na matokeo ya uchaguzi. Hata mimi, pia, zaidi kushinda ninavyweza kueleza.
"Ninajua
si jambo rahisi. Najua wiki moja iliyopita, watu wengi wamekuwa
wakijiuliza iwapo Marekani ni nchi ambayo tumekuwa tukiamini ndiyo.
"Migawanyiko iliyowekwa wazi na uchaguzi huu imekolea, lakini tafadhali nisikezi ninaposema hili.
"Marekani
ni ya thamani. Watoto wetu ni wa thamani. Kuweni na imani katika nchi
yetu, mpiganie maadili yetu na daima, msikate tamaa."
Alipokuwa anatoa hotuba ya kukubali kushindwa wiki iliyopita, Bi Clinton alsiema Bw Trump anafaa kupewa fursa ya kuongoza.
Tangu wakati huo, amekuwa haonekani, ingawa siku moja alionekana akifanya matembezi porini.
Kwenye mawasiliano ya simu ambayo yalifichuliwa kwa wanahabari
Marekani, alisikika akimlaumu mkurugenzi mkuu wa FBI James Comey,
aliyetangaza kuanzishwa kwa uchunguzi mpya kuhusu kashfa yake ya barua
pepe zikiwa zimesalia siku 11 kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika.
Baadaye
uchaguzi ulipokuwa umekaribia kabisa, Bw Comey alisema hakukupatikana
ushahidi mpya ambao ungebadilisha uamuzi wa awali wa FBI kwamba hakukuwa
na ushahidi wa kumfungulia mashtaka.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269