Jeshi la serikali ya Somalia limefanikiwa kukomboa mji wa Jouf Judud katika mkoa wa Juba ya Kati huko kusini mwa nchi hiyo.
Ripoti zinasema kuwa mapigano ya kukomboa mji wa Jauf Judud yamesababisha vifo vya watu kadhaa na kujeruhiwa wengine wengi.
Mafanikio hayo ya jeshi la Somalia yanafuatia kukombolewa kwa eneo la
kistratijia la Bakool huko kusini magharibi mwa Somalia. Eneo hilo
ambalo limekuwa likishikiliwa na wapiganaji wa kundi la kigaidi la al
Shabab lilikombolewa baada ya mapambano makali ya jeshi la Somalia
likisaidiwa na askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika (Amisom).
Hata hivyo ripoti zinasema baadhi ya vijiji na miji ya mkoa wa Juba
ya Kati vingali vinadhibitiwa na wapiganaji wa kundi la kigaidi la al
Shabab.
Jeshi la Somalia likisaidiwa na askari elfu 22 wa Umojawa Afrika
linaendelea kupambana na wapiganaji wa kundi la al Shabab hususan katika
maeneo ya kusini mwa nchi hiyo.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269