Katibu Mkuu wa Umoja w Mataifa ametoa indhari kuhusu uwezekano wa kufanyika jinai kubwa nchini Sudan Kusini.
Ban Ki moon ametoa taarifa na kutangaza kuwa kuna hatari ya
kutokea maafa makubwa Sudan Kusini na hii ni katika hali ambayo vikosi
vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa havina nyenzo zinazohitajika
kuzuia maafa hayo.
Imeelezwa kuwa kupitia ripoti ya siri aliyotoa, Katibu Mkuu wa UN
ameituhumu serikali ya Sudan Kusini kuwa imefanya uzembe na amelitaka
Baraza la Usalama la umoja huo kuunda kikosi cha nchi za eneo za kutoa
msaada kwa askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa.
Katika ripoti yake hiyo, Ban Ki moon amebainisha kuwa kuna ushahidi
unaoonyesha kuwa katika kipindi cha wiki zilizipota kumekuwepo ongezeko
la vitendo vya kufurutu mpaka na uenezaji chuki nchini Sudan Kusini na
vilevile wito wa kuzusha machafuko ya kikabila ambao unazidisha
uwezekano wa kutokea maafa makubwa.
Ripoti ya Katibu Mkuu wa UN inatolewa katika hali ambayo siku ya
Jumatatu, Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini alitangaza kuwa uvumi
ulioenezwa na baadhi ya maafisa wa serikali wa kufanyika wizi wa dola
milioni 280 katika hazina ya umma una lengo la kuchafua utendaji wa
serikali katika mazingira nyeti na hasasi ya kisiasa yaliyopo hivi sasa
nchini humo.
Ikumbukwe kuwa moja ya matatizo yanayowakabili wananchi wa Sudan
Kusini kwa sasa ni ongezeko la ukosefu wa ajira ambao kwa mujibu wa
Benki ya Dunia umefikia kiwango cha asilimia 12. Aidha raia zaidi ya
milioni nne wanakabiliwa na hatari ya baa la njaa kutokana na vita na
mapigano yaliyoikumba nchi hiyo.../
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269