Katibu
Mtendaji wa Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA), Fabian Magoma
(kulia), akizungumza katika Kongamano la 33 la siku tano la Chama cha
Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea Hoteli ya Kebby Mwenge
jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Mwenyekiti wa TPHA
anayemaliza muda wake, Daktari Bingwa Elihuruma Nangawe.
Dk. Manase Frank akitoa mada kwenye kongamano hilo.
Profesa Andrew Swai akitoa mada.
Wadau wa sekta ya afya wakifuatilia kwa karibu mada zilizokuwa zikitolewa katika kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Dk.
Andronicus Aloyce Rwelamila kutoka Hospitali ya Tumbi Kibaha (kushoto)
na Muuguzi wa Hospitali hiyo, Mary Gowele wakiwa kwenye kongamano hilo.
Kongamano likiendelea
Usikivu katika kongamano hilo. Kushoto ni Mwenyekiti wa TPHA, Dk. Elihuruma Nangawe
Profesa Japhet Kileo (kulia), akiuliza maswali kwenye
kongamano hilo.
Dk.
Mwanahamisi Magwangwara (kushoto), akizungumza wakati akijibu maswali
mbalimbali kutoka kwa wadau wa sekta ya afya katika kongamano la 33 la
siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea
Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni mtoa mada,
Profesa Andrew Swai.
Dk.Chilolo
Edward (katikati), akijibu maswali kuhusu changamoto ya waendesha
bodaboda. Kushoto ni Profesa Andrew Swai na Dk. Manase Frank.
Mkurugenzi
wa Shirika la Wanawake katika Jitihada za Maendeleo (WAJIKI), Janeth
Mawinza akielezea changamoto ya matumizi ya pombe katika Manispaa ya
Kinondoni.
Na Dotto Mwaibale
MADAKTARI nchini wametakiwa kufanya mikutano ya kijamii au wananchi ili kuwapa fursa ya kujua magonjwa yanayo wakabili.
Hayo
yalielezwa na Dk. Manase Frank wakati akitoa mada katika kongamano la
33 la siku tano la Chama cha Afya ya Jamii Tanzania (TPHA) linaloendelea
Hoteli ya Kebby Mwenge jijini Dar es Salaam leo asubuhi.
"Changamoto
kubwa tuliyonayo ni wananchi wengi kutojua magonjwa yanayowasumbua
hivyo ni muhimu kwa madakatari kuitisha mikutano itakayowakutanisha na
wananchi ili kuondoa changamoto hiyo" alisema Dk. Frank.
Alisema
wagonjwa wengi wamekuwa wakikata tamaa kwa kuchangiwa na kauli za
baadhi ya madaktari ambao wanashindwa kujua tatizo la mgonjwa husika
hivyo wakati umefika wa madaktari kushirikiana kwa karibu na jamii,
viongozi wa dini ili kuondoa changamoto hiyo.
Akitolea
mfano wa kijana mmoja ambaye alifiwa na ndugu zake wote wa karibu
kutokana na ugonjwa wa ukimwi na kuishi kwa kunyanyapaliwa lakini
baadaye afya yake ilikuja kuimarika kufuatia ushauri uliotolewa na
daktari kwa jamii iliyokuwa ikimzunguka wakati wa ugonjwa wake.
Mtoa
mada mwingine Profesa Andrew Swai aliomba serikali wakati wa siku ya
Jumamosi na Jumapili kufunga baadhi ya barabara ili zitumike kwa
wananchi kufanya mazoezi ya kutembea ili kujenga afya za miili yako na
kuepukana na magonjwa kama kisukari.
Akizungumzia changamoto ya matumizi ya bodaboda Dk.Chilolo
Edward alisema kwa mwaka jana katika Hospitali za mikoa ya Morogoro,
Tumbi Pwani na Shinyanga kulikuwa na ajali 895 huku majeruhi wakiwa
4813.
Alisema
majeruhi waliolazwa katika hospitali hizo walikuwa ni 4525, waliopewa
rufaa kwenda hospitali za Bugando na Muhimbili walikuwa 71 na waliolazwa
ni 702.
Alisema vifo vilikuwa 81 hivyo vilitokea baada ya kufikishwa Hospitalini ni 70 na vilivyotokea eneo la ajali vilikuwa 11.
Dk.Chilolo
alisema ili kupunguza changamoto hiyo inapaswa watoa huduma za afya
kutoa elimu kwa waendesha boda boda pale wanapofikishwa mahospitali
kuhusu umuhimu wao katika familia na taifa kwa ujumla hivyo kuwa makini
wanapoendesha vyombo hivyo vya moto badala ya kuacha kazi hiyo kufanywa
na polisi au Sumatra.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269