Mwenyekiti
wa Chama Cha Wauguzi Tanzania cha Akiba na Kukopa (SACCOS), Adam Leyna
(wa tatu kushoto) akifungua Mkutano Mkuu wa pili wa chama hicho
uliofanyika katika Ukumbi wa Makuti wa JKT Mgulani Dar es Salaam. Kutoka
kushoto ni, Afisa Ushirika Manispaa ya Kinondoni, Scholastica Maganga,
Afisa Ushirika Manispaa ya Kinondoni, Rosemary Mkosamali na wa kwanza
kulia ni Meneja wa Ngome Saccos, Sudi Mangara
Mshehereheshaji akiendesha Mkutano huo, ambaye ni Afisa Muuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Clauda Mlombo
Afisa Muuguzi Msaidizi wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro, Shaibu Ally akiongoza ufunguzi wa Sala katika Mkutano huo
Viomgozi wakiwa meza kuu, kunzia kulia ni, Meja, Lea Mtuma akimwakilisha Mkuu wa Jeshi la kujenga Tafa (JKT ), Meneja wa Ngome Saccos, Sudi Mangara, Mwenyekiti wa Chama Cha Wauguzi Tanzania cha Akiba na Kukopa (SACCOS), Adam Leyna, Afisa Ushirika Manispaa ya Kinondoni, Rosemary Mkosamali na Afisa Ushirika Manispaa ya Kinondoni, Scholastica Maganga
Afisa Muuguzi Mkuu Hospitali ya Lugalo, Devota Mutayoba akiongoza ibada katika mkutano huo
Muuguzi akifatilia jambo kwa umakini mkubwa
Wauguzi wakiimba wimbo wa chama chaokatika mkutano huo
Na Khamisi Mussa
MWENYEKITI
wa Chama Cha Wauguzi Tanzania cha Akiba na Kukopa (SACCOS), Adam Leyna
amewaomba wanachama ambao ni wauguzi kuchangamkia fursa ya mikopo kutoka
katika chama hicho na kuachana na kukimbilia kukopa katika mabenki
ambayo yanatoza riba kubwa.
Leyna
aliyasema hayo wakati jijini Dar es Salaam leo wakati alipokuwa
akifungua mkutano mkuu huo ambapo alitoa wito kwa wauguzi wote nchini
kujiunga na Saccos hiyo kwani ni mali yao.
"Saccos
hii ni yetu na ipo kwa sababu maalumu ya kiinua uchumi wa wanachama ili
tujikomboa na changamoto ya maisha tuliyonayo" alisema Leyna.
Leyna aliwataka wauguzi hao kuhamasishana ili kupata wanachama wengi ili kukuza chama hicho ambacho ni muhimu kwao.
Afisa Ushirika Manispaa ya Kinondoni, Rosemary Mkosamali (kulia) akimkabidhi kadi ya uanachama, Afisa Muuguzi wa Kituo cha Afya cha Kirwa Mashati kilichopo Wilaya ya Rombo Mkoa wa Kilimanjaro, Theopista Njau
Wanachama wakiserebuka
Wanachama wakiserebuka
Wanachama wakiserebuka
Afisa Ushirika Manispaa ya Kinondoni, Rosemary Mkosamali (kulia) akimkabidhi kadi ya uanachama Afisa Mfawidhi Daraja la Kwanza Hospitali ya Taifa Muhimbili, Violet Minja
Picha ya pamoja . (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269