Breaking News

Your Ad Spot

Nov 15, 2016

OBAMA : KARIBUNI HIVI TRUMP ATAKABILIANA NA UKWELI WA MAMBO KUHUSU AHADI ALIZOZITOA

Rais Barack Obama wa Marekani amemuonya rais mteule wa nchi hiyo, Donald Trump kwamba hivi karibuni atashuhudia ukweli wa mambo juu ya utekelezaji wa ahadi zake tata alizozitoa kwa Wamarekani wakati wa kampeni.
Obama ameyasema hayo huko Athes Ugiriki katika kikao cha kwanza na waandishi wa habari baada ya uchaguzi wa rais nchini humo ambapo amemuonya rais huyo mteule juu ya kutotekeleza ahadi hizo.
Uhalisia wa mvutano wa kisiasa unaotawala hivi sasa Marekani
Ameongeza kuwa, ahadi tata za Trump alizozitoa kwenye kampeni kukiwemo kuwafukuza mamilioni ya wahajiri, kuvunja makubaliano ya kiulinzi baina ya Marekani na Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi NATO, makubaliano ya nyuklia baina ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kundi la 5+1, kuwazuia Waislamu kuingia Marekani na kujenga ukuta ili kuwazuia raia wa Mexico kuingia nchini humo, ni mambo ambayo kutekelezwa kwake ni kugumu kuliko kuyatamka tu. Lengo la matamshi hayo ya Obama ni kuzitoa wasi wasi nchi za Ulaya kuhusiana na misimamo ya Donald Trump.
Maandamano ya kumpinga Trump yanaendelea
Akiwa katika safari yake ya mwisho nje ya nchi, Rais Obama anatazamiwa kukutana na viongozi wa nchi za Jumuiya ya Ulaya na kuwapa matumaini kwamba Washington itaendelea kutekeleza sera za kudumisha ushirikiano na nchi hizo. Hii ni katika hali amabayo kabla ya hapo Rais Barack Obama alionya kwamba Trump hana shakhsia ya kuwa rais wa Marekani. Ushindi wa Trump katika uchaguzi wa tarehe 8 mwezi huu, umeibua hali ya wasi wasi mkubwa kwa viongozi wote wa dunia kutokana na misimamo yake hasi.
Sehemu nyingine ya maandamano dhidi ya Trump
Kufuatia hali hiyo, maelfu ya raia wa Marekani wameendelea kufanya maandamano katika miji mingi ya nchi hiyo kulalamikia kile wanachosema ni ukandamizaji wa thamani za demokrasia.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages