Breaking News

Your Ad Spot

Nov 14, 2016

RAIS WA SOMALIA: MAENEO MENGI YA NCHI YANAKABILIWA NA UKAME

Rais Hassan Sheikh Mohamoud wa Somalia ameitaka jamii ya kimataifa kutuma misaada ya dharura katika maeneo yanayokabiliwa na ukame na baa la njaa nchini humo.
Rais huyo amewataka Wasomali waishio nje ya nchi kuwajali ndugu zao wanaokabiliwa na njaa na kiu kutokana na ukame unaoitafuna nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
Rais wa Somalia amesema msimu wa masika umepita pasina kushuhudiwa mvua zozote nchini humo, hivyo maeneo mengi yanakabiliwa na ukame. Ameitaka jamii ya kimataifa kuingilia kati na kutuma misaada ya dharura katika maeneo hayo kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Taathir hasi za ukame Somalia
Mwanzoni mwa mwaka huu, wataalamu walionya kwamba mwaka huu wa 2016 utashuhudia ukame katika baadhi ya nchi za Afrika hususan eneo la Pembe ya Afrika. Taathira hasi za El-Nino  sambamba na ukame na mafuriko katika nchi za Somalia na Ethiopia zimeyaweka hatarini maisha ya watu wengi wa nchi hizo.
Ofisi ya Uratibu Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa mwezi Septemba mwaka huu ilisema kuwa, uhaba wa maji katika nchi za Somalia na Ethiopia umesababisha karibu watoto milioni tatu kukumbwa na hatari ya utapiamlo, huku karibu raia milioni tano wa Somalia wakihitaji misaada ya chakula.
Mbali na majanga hayo ya kimaumbile, Somalia inakabiliwa na harakati za kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab ambalo limekuwa likitekeleza mashambulizi ya kigaidi kila leo.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages