Rais mteule wa Marekani Donald Trump
aliwashangaza wateja, na wanahabari wanaofuatilia safari zake, baada ya
kujitokeza kwa kushtukiza katika mgahawa mmoja New York.
Wanahabari
waliopewa kazi ya kufuatilia safari zake walibaki kushangaa kwani
walikuwa wameelezwa kwamba angesalia nyumbani jioni hiyo.
Lakini
badala yake, aliandamana na kundi ndogo la maafisa hadi kwenye mgawaha
wa 21 Club katika mtaa wa Manhattan, mmoja wa migahawa anayoipenda sana.
Video
zilizopigwa wakati wa kisa hicho Jumatano zinamuonyesha Bw Trump
akiwasalimia wateja na kuwaambia kwamba atapunguza kodi wanayolipa kwa
serikali.
Kuwasili kwake 21 Club kulijulikana baada ya mwandishi
wa Bloomberg, Taylor Riggs, ambaye kibahati alikuwa ameenda kwenye
mgahawa huo, alipakia kwenye Twitter ujumbe wa kusema kwamba Trump
alikuwa amefika kwenye mgahawa huo. Hata hivyo, alikosea jina la eneo na
badala yake akasema ilikuwa ni Keene.
Kwneye video, Bw Trum anaonekana akiwaambia wateja: "Tutapunguza kodi mnayolipa, msiwe na wasiwasi kuhusu hilo."
Kundi
la wanahabari waliopewa kazi ya kufuatilia safari za rais huyo mteule,
inadaiwa waliambiwa na msemaji wa Bw Trump, Hope Hicks, mwendo wa saa
18:45 kwamba alikuwa amekamilisha shughuli za siku na kwamba walikuwa
huru kwenda nyumbani.
Dakika 45 baadaye, msafara mkubwa wa magari
ulionekana ukiondoka kutoka afisi kuu ya Bw Trump kwa sasa katika jumba
la Trump Tower. Msafara huo ulijumuisha magari zaidi ya kumi na gari la
kubeba wagonjwa.
Riggs alipoandika kwenye Twitter, wanahabari walikimbia mgahawa wa Keene kabla ya kugundua kwamba alikuwa 21 Club.
Hawakuruhusiwa
kuingia Trump na familia yake walipokuwa wanakula chakula cha jioni
kabla ya kiongozi huyo kuondoka na kurejea Trump Tower saa 21:41.
Hatua ya kutofuata desturi na kutowafahamisha wanahabari
wanaomfuatilia rais mteule kuhusu safari hiyo imevitia hofu vyombo vya
habari Marekani
Vyombo hivyo tayari vina wasiwasi kuhusu kunyimwa
uhuru wa kufikia na kuzungumza na maafisa wa Bw Trump, na uwezekano wa
kuzuiwa kupata habari zautawala wake kwa urahisi atakapoingia
madarakani.
Bi Hicks baadaye aliwaambia wanahabari kwamba
hakufahamu mipango ya Bw Trump na akaahidi kwamba wanahabari "watapata
uhuru wa kufikia maafisa wa serikali na taarifa za serikali kama
ilivyokuwa chini ya marais wengine".
Chama
cha Waandishi wa Habari wa Ikulu ya White House kimeshutumu kisa hicho.
Viongozi wa chama hicho wamesema "haikubaliki kwa rais ajaye wa
Marekani kusafiri bila waandishi wa habar wa kufuatilia habari zake na
kuwafahamisha wananchi kuhusu alipo".
Rais wa chama hicho Jeff
Mason hata hivyo amesema amepokea hakikisho kutoka kwa Bi Hicks lakini
akasema wakati wa kutekeleza ahadi hiyo ni sasa na kusisitiza kwamba
"waandishi wa habari wa kumfuatilia rais mteule wapo...kufuatilia
shughuli zake anapoandaa serikali mpya".
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269