Rais-mteule wa Marekani Donald Trump
amewateua watu wenye chuki na Uislamu kuhudumu katika Ikulu ya White
House jambo linaloashiria muendelezo wa sera zake za chuki ambazo
zimewatia hofu Waislamu nchini humo.
Ijumaa mashirika ya kijamii na viongozi wa Waislamu Marekani
walitangaza bayana wasiwasi wao kuhusu hatua ya Trump kuwateua watu
wenye chuki na Uislamu katika nyadhifa muhimu za usalama wa taifa.
Hata baadhi ya maafisa wa serikali ya sasa na zilizopita
Marekani wamebainisha wasi wasi wao kuwa watu walioteuliwa na Trump
wataupa nguvu mtazamo wa Waislamu kuwa Marekani inaendesha vita dhidi ya
dini ya Uislamu. Tokea Trump atangazwe mshindi katika uchaguzi wa rais
wa Marekani, kumeshuhudiwa wimbi la hujuma dhidi ya Waislamu na watu wa
jamii za wachace nchini humo.
Ijumaa, afisa mstaafu katika Jeshi la Marekani Luteni Jenenrali
Michale Flynn alikubali uteuzi wa Trump wa kuhudumu kama mshauri wa
usalama wa taifa. Flynn ana historia ya kutoa matamshi makali dhidi ya
Uislamu. Naye Seneta Jeff Session amekubali uteuzi wa Trump wa kuwa
mwanasheria mkuu Marekani. Seneta huyo anaunga mkono kauli ya Trump ya
kutaka kuzuiwa Waislamu kuingia Marekani. Aidha Trump amemteua mjumbe wa
Congress, Mike Pompeo kuwa mkuu wa Shirika la Ujasusi la Marekani, CIA.
Pompeo amekuwa akitoa madai kuwa viongozi wa Waislamu Marekani
hawachukui misimamo imara dhidi ya ugaidi. Halikadhalika anapinga vikali
mapatano ya nyuklia baina ya Iran na madola sita makubwa duniani.
Ibrahim Hooper, Msemaji wa Baraza la Mahusiano ya Uislamu na Marekani
CAIR amesema ni jambo la kushangaza kuona watu wenye chuki na Uislamu
wakipewa nafasi muhimu katika serikali ya Trump.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269