Breaking News

Your Ad Spot

Nov 19, 2016

UISLAMU SIO UGAIDI ASEMA DC MONDULI

1
Na Mahmoud Ahmad Arusha
SERIKALI imesema Uislamu sio ugaidi hivyo dini isihusishwe na ugaidi na wala Uislamu usitumike kama ngao ya kufanya uhalifu bali ugaidi ni uhalifu na atakaejihusisha na ugaidi ashughulikiwe kama wahalifu wengine .
Yameelezwa jana na mkuu wa mkoa wa Arusha ,Mrisho Gambo, kwenye kongamano la Kiislamu lililoandaliwa na Marakazi ya Al Azhar Sharif, Changombe ,Dar Es Salaam, lililofanyika ukumbi wa ccm, mkoa wa Arusha, lililokuwa likizungumzia athari za Fatua zinazohalalisha umwagaji wa damu zilizohifadhiwa na kutyumbisha amani na utulivu.
Kwenye hotuba hiyo iliyosomwa na mkuu wa wilaya ya Monduli, Iddy Kimanta, amesema vipo vitendo vingi vinafanywa na baadhi ya watu kwa kisingizio cha dini ya Kiislamu jambo ambalo sio sahihi hatakidogo kwa kuwa dini inakataza kumwaga damu au kuua nafsi isiyo kuwa na hatia .
Akasema wanaojihusisha na ugaidi watashughulikiwa kama magaidi na kamwe wasihusishwe na uislamu kwa kuwa dini haina uhusiano wowote na ugaidi.KUhusu elimu, Kimanta,amewataka wazazi kuhakikisha wanasomesha watoto wao elimu zote mbili ya Dunia na Akhera, na hivyo kuwajenga kwenye malezi yaliyo bora ambayo yana maadili ya uislamu.kwa kuwa yatawawezesha kujiepusha kujiingiza kwenye uhalifu na ugaidi.
”Arusha ni eneo lipo kwenye hatari zaidi kwa kuwa tunakaribiana na maeneo ambayo kama kama vijana wasipopelekwa kwenye malezi yenye maadili watatumika kwenye ugaidi ,mfano anakuja mtu anachukua vijanakwa madai anawapeleka nje kusoma na mzazi hahoji mtoto wake anaenda kusoma kitu gani ”alisema, kimanta.
AmeseKUhusu matumizi ya mitandao, amesema ipo mitandao mingi lakini sio yote yenye nia njema na Uislamu hivyo wazazi lazima wawe makini kwa kuwa mitandao mingi inalenga kuvuruga na kuwagawa na hatimae ni kuporomoka kwa maadili katika jamii.
Amesema kibaya zaidi wazazi nao wanatumia muda mwingi kwenye mitandao na hivyokusahau majukumu yao ya malezi na mitandao ina nguvu kubwa kuliko Quraan tukufu na hivyo sasa wazazi na watoto wanaishi kimtandao tandao badala ya kusomesha watoto ili wapate elimu yenye manufaa.
Awali Shekhe wa mkoa wa Arusha, Shaaban bin Jumaa, amesema hivi sasa kuna vikundi vingi vimezuka ambavyo vinakuwa vikitoa Fatua(MATAMKO) juu ya dini ambayo yanapotosha na kusababisha mitafaruku na migogoro .Amesema Fatua inatakiwa kutolewa na kiongozi mwenye elimu kubwa aliyebobea kwenye dini na sio hali ilivyo ambaposasa mtu yeyote ambae hana elimu kubwa wala sio kiongozi anatoa fatua.
Amesema kinachosababisha hayo kutokea ni kutokuheshimiana ambapo kila mmoja sasa anataka madaraka wakatihana sifa hiyo hivyo kilichopo ni kila mmoja kumheshimu mwingine aliyemzidi elimu ya dini na hivyofatua zittaondoka.
Amesema elimu ndogo ndio inayopelekea watu kufanya vitendo vya ugaidi na kusingizia dini wakidai ni jihadi jambo ambalo sio sahihi hata kidogo.(P.T)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages