Mkurugenzi
Idara ya Katiba na Ufuatiliaji Haki Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria
Bw. Patience Ntwina (aliyesimama) akitoa taarifa ya utekelezaji wa
Miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa ujumbe wa
wataalam kutoka Umoja wa Mataifa waliotembelea Wizarani hapo leo
(14/11/2016).
Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Nchi Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa
Umma na Utawala Bora Zanzibar Bw. Kubingwa Mashaka Simba akitoa taarifa
ya utekelezwaji wa miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa ujumbe
wa wataalam wa Umoja huo waliotembelea Wizara ya Mambo ya Katiba na
Sheria Tanzania Bara leo (14/11/2016) jijini Dar Es Salaam. Ujumbe huo
umeahidi kuendelea kufadhili miradi mbalimbali baada ya kuridhiswa na
utekelezwaji wake.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akiongea
katika kikao na wataalam mbalimbali kutoka ujumbe wa Umoja wa Mataifa
ambao wametembelea Wizarani hapo leo (14/11/2016) ili kujionea namna
Wizara hiyo ilivyofaidika na kutekeleza miradi mbalimbali inayofadhiliwa
na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa. Wananchi hasa wasiojiweza
wameweza kupata haki zao kupitia miradi hiyo.
Sehemu ya
wataalam kutoka ujumbe wa Umoja wa Mataifa waliotembelea Wizara ya
Mambo ya Katiba na Sheria wakiwa katika kikao na Katibu Mkuu wa Wizara
hiyo ( hayupo pichani) ili kuona namna miradi inayofadhiliwa na Umoja
huo inavyotekeleza. (P.T)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269