Breaking News

Your Ad Spot

Nov 18, 2016

VIJANA WAMUWEMA NJIAPANDA AFISA MAENDELEO KIGOMA

 NA MAGRETH MAGOSSO,KIGOMA

WANANCHI  wa Manispaa ya kigoma Ujiji wameshangazwa na kitendo cha ofisa maendeleo wa vijana mkoani humo Edward Manase  kushindwa kujibu hoja ya asilimia tano ya vijana kuwekezwa  katika moja ya mfuko wa hifadhi ya jamii, ilihali  hawajajiunga na mfuko huo(PSPF).

Hoja hiyo ilitolewa na mmoja wa wanakamati kutoka Kata ya Bangwe Anatoria Cronery  jana kwenye mafunzo ya kamati za kata tisa zilizopo katika mradi wa uwazi,uwajibikaji ,mgawanyo wa rasilimali na mapambano dhidi ya rushwa uliolenga kubainisha fursa za kata,matatizo na namna ya kuzipatia ufumbuzi,uliodhaminiwa na Asasi ya kiraia ya Nyakitonto Youth For Development Tanzania.

Awali  Ofisa vijana Mkoa  Edward Manase akiwasilisha mada ya fursa ya vijana na mpango kazi ambapo alisema  asilimia tano za vijana inakabiliwa na changamoto ya kutokuwa  na vikundi endelevu kwa kuwa vikundi vingi ni vya msimu tu,

Manase alisema ili kukabilina na hilo mkoa umeandaa mpango wa mitaji/nyenzo za miradi,mafunzo ya stadi kazi,kwa lengo la kupunguza umaskini na utegemezi kwa familia zao hali inayochangiwa na vijana wengi wanapenda shughuli za kupata fedha kwa haraka ,ilihali kuna sekta ya kilimo kupitia ardhi iliyopo.

Akiomba ufafanuzi wa mada wasilishwa Anatoria Cronery alihoji mitaji yao kwa maana ya asilimia tao za vijana kuwekezwa katika mfuko wa hifadhi ya jamii ya PSPF bila kuwa wanachama wa mfuko huo,kwa kuwa wengi wameshindwa kujiunga kutokana na ukosefu wa ajira ya kulipa ada ya sh.20,000 kila mwezi ili wanufaike na huduma ya Bima ya Afya.

Cronery alisema inashangaza kuingiziwa fedha za kuwakopesha vijana ili wajikwamue kiuchumi badala yake wanawekeza katika mfuko huo bila kufahamishwa wananufaikaje na rasilimali fedha hiyo,ilihali hawana vigezo vya kunufaika na asilimia tano hiyo.

Ajabu ofisa huyo alishindwa kutoa majibu ya papo kwa hapo kwa mujibu wa mada yake badala yake alisema shughuli zote za kurasimisha vikundi na utoaji wa fedha hizo zinafanyika katika halmashauri husika na mkoa unasimamia  tu,hivyo ni ngumu kujua vikundi hai na shughuli zingine za vijana.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa mafunzo hayo Girbert  Kusongwa alishauri watumishi  na wataalamu wa idara za umma wajitambue ,wasipende kukaa ofisini vikundi vingi kuundwa wakati wa ujio wa mwenge na si kuwainua vijana lengwa kwa mujibu wa serikali kuu.

Akifunga mafunzo hayo ya siku moja Mratibu wa asasi hiyo Joel Ramadhan alisema watendaji wa kata na wenyeviti wake wahakikishe wanaweka mabango yenye kuonesha rasilimali zilizopo katika kata ,vikwazo vya rasilimali na ufumbuzi na kuandaa taarifa ya utekelezaji wa mradi ili wnanachi wajue fursa na kuzitumia.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages