Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kwa
Spika Mstaafu, Samuel Sitta, bungeni mjini Dodoma, Novemba 11, 2016. (PICHA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU)
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa
(wapili kulia) akimfariji mjane wa Spika Mstaafu Mama Margareth Sitta
baada ya mwili wa Spika Mstaafu, Marehemu Samuel Sita kuwasili kwenye
uwanja wa ndege wa Dodoma
Jeneza lenye mwili wa Spika Mstaafu, Samuel Sitta ukiingizwa
bungeni mjini Dodoma
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID
WABUNGE wa bunge
la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Novemba 11, 2016, wamebubujikwa na
machozi, wakati jeneza lenye mwili wa marehemu Samwel Sitta, “Mzee wa Kasi na
Viwango” lilipowekwa kwenye jengo la bunge ili kutoa fursa ya wabunge kutoa
maelezo ya kumbukumbu ya Mzee Sitta na kisha kutoa heshma za mwisho.
Miongoni mwa
wabunge walioshindwa kujizuia wakati akiomba dua, ni Waziri wa Sheria na
Katiba, Dkt. Harrison Mwakyembe, ambaye pamoja na mambo mengine, kupitia maombi
hayo alimwelezea spika Sitta kwamba alikuwa ni mtu mwenye msimamo na
anayeipenda nchi yake na kuwapenda wanyonge lakini akichukizwa na “walafi”
mafisadi.
Naye Kiongozi wa
chama cha ACT Wazalendo, na Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe, aliwataka
wabunge na watanzania kwa ujumla kumuenzi Mee Sitta kwa vitendo, ambapo katika
uongozi wake kama spika wa bunge la 9, alifanya mageuzi makubwa ya muundo wa
bunge na utendaji kazi wake.
Akiongea kwa
niaba ya Chadema, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, alimwelezea
marehemu Sitta kama kiongozi aliyetoa fursa kwa demokrasia kuchanua.
Naye Kiongozi wa
kambi rasmi ya upinzani bungeni, Freeman Mbowe, aliwataka wabunge kudumisha
upendo na heshima miongoni mwao bila ya kujali itikadi zao za vyama, na
kubainisha kuwa wapinzani hawakumuelewa Mzee Sitta kama kweli ni mwana CCM kwa
jinsi alivyowapa fursa ya kuzungumza bungeni na hata wakati mwingine
kuwalazimisha mawaziri kujibu maswali kwa ufasaha.
Akizungumza kwa
niaba ya wabunge wa CCM, Mh. Jason Rweikiza alimuelezea maehemu kuwa alikuwa ni
mwana CCM mwaminifu aliyesaidia kukijenga chama na kukipatia heshima kubwa
kutokana na uongozi wake imara.
Naye waziri Mkuu
Kassim Majaliwa, alisema serikali ilipokea kwa mshtuko mkubwa kifo cha marehemu
Mzee Samwel Sitta, na mchango wake katika utumishi wa umma kamwe
hautasahaulika.
Naye Spika wa
bunge Job Ndugai, alimsifu marehemu kuwa hakuwa mtu mchoyo, aliwezesha kukuza
vipaji vya wale waliokuwa chini yake na kutolea mfano yeye mwenyewe ambaye sasa
ni spika kutoka nafasi ya uenyekiti wa bunge wakati wa uongozi wa marehemu
Sitta, lakini pia Spika wa sasa wa bunge la Zanzibar na Waziri wa Nchi Ofisi ya
Waziri Mkuu, (Sera na watu wenye ulemavu), Mh. Jenista Mhagama ni miongoni mwa
mafanikio ya Marehemu Sitta.
Akitoa wasifu wa
marehemu, naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson, alisema, marehemu Sitta alizaliwa tarehe
18/12/1942 huko Urambo mkoani Tabora, alipata elimu ya msingi mwaka 1950 katika
shule ya msingi Urambo kabla ya kuahamia shule ya msingi Sikonge (Middle
School), kutoka mwaka 1954 hadi 1957.
Marehemu Sitta,
alijiunga na shule ya sekondari ya wavulana, Tabora Boys, mwaka 1958 alisoma
kidato cha kwanza hadi cha sita na kuhitimu mwaka 1963.
1964 Marehemu
alijunga na chuo kikuu cha Dar es Salaam ambako alisomea shahada ya sheria na
kuhitimu mwaka 1971. Baada ya hapo alijiendeleza kielimu kwenye vyuo mbalimbali
vya ndani na nje.
Marehemu
alifanya kazi mbalimbali serikalini na kwenye chama.
Marehemu ameacha
mjane na watoto watano.
Marehemu Mzee
Samwel Sitta, kama anavyojulikana kwa jina la Mzee wa “Kasi na Viwango” au
Chuma cha Pua, anatarajiwa kuzikwa nyumbani alikozaliwa, huko Urambo, Jumamosi
Novemba 12, 2016.
Mungu ailaze
roho ya marehemu mahala pema peponi AMIN.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika
kikao maalum cha bunge cha kumuenzi Spika Mstaafu, Samuel Sitta, bungeni mjini
Dodoma Novemba 11, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
akimfariji mjane wa Spika Mstaafu Mama Margareth Sitta baada ya mwili wa
Spika Mstaafu, Marehemu Samuel Sitta kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma
Waziri Mkuu Mstaafu, Samuel Malecela akimpa pole
mjane wa Spika Mstaafu, Margareth Sitta bungeni mjini Dodoma
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka shada la
maua kwenye jeneza la Spika Mstaafu Samwel Sitta, bungeni mjini Dodoma
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Spika wa Bunge,
Job Ndugai pamoja na viongozi wengine wakiusubiri mwili wa Spika mstaafu,
Samuel Sitta uteremshwe kwenye ndege katika uwanja wa ndege wa Dodoma Novemba
11, 2016
Mwili wa Spika Mstaafu Samuel Sitta ukiteremshwa
kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma Novemba 11, 2016
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269