Mamilioni ya watu wanashiriki katika
matembezi ya kumbukumbu ya Siku ya Arubaini ya Imam Hussein AS ambapo
pia wanatia saini waraka wenye ujumbe unaofafanua kuhusu mjumuiko huu
mkubwa zaidi duniani.
Washiriki wa matembezi hayo ya Arubaini ya Imam Hussein AS
katika njia ya kutoka Najaf hadi Karbala Iraq wameandika barua kwa
walimwengu na kueleza kuhusu hali ya leo duniani inayokwenda kwa mujibu
wa maslahi ya madola ya kiistikbari na wanaoleta hitilafu baina ya
mataifa na watu wa rangi mbali mbali. Kwa msingi huo washiriki wa
matembezi hayo wametoa wito kwa watu wa nchi mbali mbali duniani
kupambana na dhulma.
Wanaoshiriki katika matembelzi hayo ya Arubaini ya Imam Hussein AS
kutoka Najaf hadi Karbala aidha wamesisitiza kuhusu kuunga mkono
wanaodhulumiwa na kupambana na dhulma.
Ujumbe huo hadi sasa umetiwa saini na maelfu ya wafanyaziara na inatabiriwa kuwa zaidi ya watu milioni moja watautia saini.
Matini ya barua ya washiriki wa matembezi ya Arubaini ya Imam Hussein
AS imeandikwa kwa lugha sita za Kiarabu, Kifarsi, Kiurdu, Kituruki,
Kiingereza na Kifaransa na iko chini ya anuani ya ArbaeenLetter katika
mitandao ya kijamii.
Maafisa wa serikali ya Iraq wanatabiri kuwa watu zaidi ya milioni 20
watashiriki katika matembezi ya Arubaini ya Imam Hussein AS mwaka huu.
Inafaa kukumbusha hapa kuwa, matembezi, majlisi na ziara ya siku ya
Arubaini hufanyika kila mwaka tarehe 20 Safar, kwa mujibu wa kalenda ya
Hijria Qamaria, baada ya kupita siku Arubaini tangu tarehe 10 mwezi wa
Muharram kwa ajili ya kukumbuka kuuawa shahidi mjukuu wa Mtume SAW, Imam
Hussein AS na masahaba zake ambao walijitolea roho zao kwa ajili ya
kuhuisha dini ya Mwenyezi Mungu katika jangwa la Karbala.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269