Breaking News

Your Ad Spot

Nov 19, 2016

ZIARA YA MAKONDA WILAYA YA KIGAMBONI LEO. ACHARUKA WATENDAJI KUTOWAJIBIKA, APIGA MARUFUKU MACHIMBO YA KOKOTO MJIMWEMA

 Mkuu wa mkoa w Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na watendaji mbalimbali Ofisini kwake, kabla ya kuanza ziara ya kukagua na kusikiliza kero za wananchi katika wilaya ya Kigamboni, leo
 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Salum Ali Hapi akisalimiana na Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro, wakati wakijiandaa kuungana na Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, kwenye ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika wilaya ya Kigamboni, leo
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaan, Paul Makonda akilakiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Mgandilwa, alipowasili kuanza ziara ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika wilaya hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Temekei, Sikunjema Yahya
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akimsalimia Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Temeke Sikunjema Yahya
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aisalimiana na Mbunge wa Kigamboni Dk Faustine Ndungulie, alipowasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Kigamboni
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akisalimia wazee maarufu alipowasili Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni leo
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akimsalimia Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Sipora Liana, alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni leo
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akisaini kitambu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, leo
  Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akisaini kitambu cha wageni katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, leo. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya hiyo Hashim Mgandilwa
 Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandilwa akimpa maeleezo Makonda
 Makonda akikagua baadhi ya ofisi kwenye jengo la Mkuu wa wilaya ya Kigamboni, Hapa huypo katika Ofisi ya DAS
 Makonda akipata maelezo kwenye chumba cha mtandao wa mawasiliano ya Internet kweye Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kigamboni 
 Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandilwa akimpa maelezo Makonda kuhusu madhari ya Ofisi yake. 
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiongozana na Mkuu wa wilaya ya Kigamboni kwenda kwenye kikao katika hotel ya Sunrise
 Ofisa Tawala wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni, Cosmas Hinju akiandaa ukumbi
 Viongozi ukumbini
 Dk Ndugulile akiwa na DAS wa wilaya ya Kigamboni Lahel Mhando
 Ukumbini
 kumbini
 Baadhi ya viongozi waalikwa wakiwa ukumbini
 Viongozi na wazee walikwa wakiwa ukumbini
 Wazee waalikwa wakisalimia

 DC wa Kigamboni akitoa maelezo ya utangulizi 
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na watendaji wa wilaya ya Kigamboni, leo, ambapo amewataka kuhakikisha kila mmoja anafanya kazi kwa ufanisi katika nafasi yake.
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikabidhiwa machapisho ya mkakati wa utendaji kazi wa Halmashauri ya Wiaya ya Kigamboni wakati wa kikao hicho na watendaki, Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya hiyo Stven Edwrd na katikati ni Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Hashim Mgandirwa 
 Makonda akitazama kwa makini kitabu cha mkakati huo baada ya kukabidhiwa. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Kigamboni HashimMgandirwa
MACHIMBO YA KOKOTO
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiingia kwenye maporomoko yaliyosababishwa na uchimbaji kokoto katika eneo la Mjimwema, Wilaya ya Kigamboni. ambapo amepiga marufuku uchimbaji huo ili kuokoa mazingira
 Mkuu wa mkoa Paul Makonda akimuonyesha mkuu wa wilaya ya Kigamboni nyumba ziliomo katika hatari ya kuporomoka kutokana na machimbo ya kokoto katika eneo la Mjimwema.
 Machimbo yaivyoadhiri ardhi
 Mkuu wa mkoa Paul Makonda akizungmza na waandishi wa habari baada ya kukagua hali kwenye machimbo hayo
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza jambo na Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dae es Salaam, Simon Sirro, wakati akikagua macho. Katikati yao ni Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Hashim Ngandirwa
NYUMBA YA WALIOATHIRIKA  KWA URAIBU
 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akipokewa alipowasili kituo cha kurekebisha waathirika wa dawa za kulevya kilichopo Vijibweni Kigamboni
 Kijana wa kituo hicho akisoma risala
 Makonda akimpa pole mmoja wa vijana wanarekebishwa katika kituo hicho
 Makonda akizungumza na vijana wa kituo hicho
 Mtu mmoja aliyeko kwenye kituo cha kurekebisha waathirika wa dawa za kulevya, kilichpo Vujibweni Kigamboni, akionyesha tumbo lake lilivyobaki na makovu ya kutisha kutokana na operesheni aliyofanyiwa kutolewa dawa za kulenya tumboni
 burudani
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Kigamboni mwishoni mwa ziara yake leo.PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO, Mtandao kwa hisani ya TTCL

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages