Meya
mteule wa manispaa ya Kigamboni mhe. Maabadi Sulemani Hoja aliye simama
akitoa neno la shukrani baada ya kuchaguliwa kuwa Meya.
Na John Luhende mwambawahabari
Uchaguzi wa Meta na Naibu Meya wa manispaa ya Kigamboni umefanyika kwa amani na utulivu ambapo wagombea wa chama cha Mapinduzi CCM wameibuka na ushindi wa nafasi zote mbili.
Uchaguzi wa Meta na Naibu Meya wa manispaa ya Kigamboni umefanyika kwa amani na utulivu ambapo wagombea wa chama cha Mapinduzi CCM wameibuka na ushindi wa nafasi zote mbili.
Akitangaza
matokeo ya uchaguzi huo mwenyekiti wa uchaguzi huo ambaye pia ni
katibu Tawala wa Wilaya ya Kigamboni Rahel Muhando amemtangaza Diwani wa
kata ya Pembamnazi
Mhe. Maabadi Suleiman Hoja (CCM) kuwa mshindi wa kiti cha Meya baada ya kupata kura 9 na kumshinda Mgombea Celestine Maufi wa CHADEMA aliye pata kura 5 kati ya kura zote 15 ambapo Kura moja iliharibika.
Mhe. Maabadi Suleiman Hoja (CCM) kuwa mshindi wa kiti cha Meya baada ya kupata kura 9 na kumshinda Mgombea Celestine Maufi wa CHADEMA aliye pata kura 5 kati ya kura zote 15 ambapo Kura moja iliharibika.
Kwa
upande wa nafasi ya Naibu meya Mhe. Amin Mzuri Sambo Diwani wa kata
Kibada ameshinda nafasi hiyo baada ya kupata kura 10 na kumbwaga
mpinzani wake Mhe. Ernest Mafimbo (CUF) aliyepata kura 5 katiya kura
zote 15 zilizopigwa.
Akizungumza
baada ya kutangazwa mshindi Meya mteule Maabadi Selemani hoja
amewashukuru wapigakura wote walioshiriki uchaguzi huo na ameahidi
kufanya kazi kwa ushirikiano bila ubaguzi wa vyama ili kuleta Maendeleo
kwa wananchi wa Kigamboni.
Naye
aliye kuwa mgombea wa nafasi ya Naibu Meya kwa upande wa UKAWA
akiwakilisha Chama Cha wananchi CUF, Ernest Ndamo Mafimbo , ameuelezea
uchaguzi huo kuwa. Ulikuwa huru na haki nakukubali kushindwa nakuahidi
kushirikiana na washindi hao ili kuwa tumikia wananchi.
“Tumekubali
wenzetu wameshinda maana hata idadi yetu sisi ilikuwa ndogo wao
wlikuwa 10 na sisi tulikuwa 5 tu kwa hiyo unaweza kuona jinsi mambo
yalivyokuwa ”
Mbunge wa
Kigamboni Dr Faustine Ndungulile , akizungumza na waandishi wa habari
baada ya kumalizika kwa uchaguzi amesema nimuda Sasa wakufanyakazi kwa
kuwa mambo mengi yalisimama kwa muda mrefu kwa kukosa baraza la
madiwani kwa kwaajili kupitisha mipango na miradi mbalimbali ya
Maendeleo.(P.T)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269