Breaking News

Your Ad Spot

Dec 18, 2016

KANISA LA AICT YATUMIA MILIONI 6 ZAWADI ZA KRIMASS KWA WATOTO YATIMA MKOANI KIGOMA

NA MAGRETH  MAGOSSO,KIGOMA
KITUO  Cha Huduma ya Mtoto (TZ973) Cha  Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT ) lililopo  katika Manispaa ya Kigoma Ujiji  kwa kushirikiana na Shirika la COMPASSION  Taifa wametumia kiasi cha Fedha  Sh.Milioni  6  kwa ajili ya zawadi za Krixmas  kwa  watoto 230 ambao ni Yatima na walio katika mazingira Magumu.

Hayo yalifahamika juzi  kigoma ujiji  katika hafla fupi ya ugawaji wa zawadi hizo sanjari na kuadhimisha miaka mitatu ya utendaji kazi wa kituo hicho tangu kuanzishwa kwake ambapo kimesaidia kuokoa maisha ya watoto  320 wanaoishi katika maisha duni na hatarishi, wakiwemo yatima ambao wengi hunyanyapaliwa  na walezi wao hasa kwa malazi,chakula,elimu,afya kitendo kinachopelekea ongezeko la watoto waishio mitaani ambapo wengi huishia kwenye makundi ya kihalifu.

Akithibitisha hilo mbele ya JamboLeo Mkurugenzi wa Kituo hicho Robert Chamungu alisema  kulea watoto yatima ni sehemu ya upendo wa Bwana Yesu Kristo,ambapo alisema wacheni watoto wadogo waje kwangu,kwa kauli hiyo imemsukuma kushirikiana na Shirika la huduma kwa watoto Nchini la COMPASSION ili kuwatimizia  ndoto zao siku za usoni.

“shirika kwa kushirikiana na kanisa wanaratibu huduma za msingi kwa watoto wa kituo hicho kuanzia elimu,afya,malazi,chakula na mavazi kwa ujumla ,kuna watoto walikuwa wanalala chini kwa walezi wao,mfadhili aliwapatia magodoro na leo tumewapa mchele kilo 5,maharagwe,kilo 3,mafuta lita 12,chumvi pakti 2 kwa kila mtoto lakini jamii iwajibike isiwachie wafadhili tu “ alieleza Chamungu.

Alifafanua kuwa kituo kina watoto 320 lakini  watoto 196 ndio wamepata wafadhili wa kuwahudumia kwa kila hitaji la msingi ambapo katika msimu wa sikukuu ya kuzaliwa Yesu Kristo baadhi yao walitumiwa zawadi za moja kwa moja na watoto 34 wanasimamiwa  kihuduma na kanisa katika kufanikisha ndoto zao siku zijazo .

Alisema jamii iwachukulie watoto yatima ni sehemu ya ibada kwa kuwalinda kwa hali na  mali kama wanavyowafanyiwa watoto wao,ambao wanatumia walichonacho bila kuwabagua na iwe hivyo kwa yatima ambao ni watoto wa ndugu na jamaa zao,wasitegemee kufeadhiliwa  siku zote kwa kuwa ufadhili una ukomo wake,hivyo jamii ikubali kubadilika kifikra.

Chamungu alieleza kuwa ifikapo mwanzoni mwa mwaka 2017 wana program ya kuwapatia mafunzo ya ujasiliamali kwa  walezi na wazazi wa watoto husika,ili kuwajengea uwezo wa kuwahudumia kwa lengo la kuwaratibu watoto wengine wenye hitaji kama hilo na watakagua kaya za walezi ,ili kutathimini  hali ya uchumi baada ya uwezeshaji wao tangu wapewe huduma  kutoka kwao.

Baadhi ya wazazi waliongea na Gazeti hili Jamila Masoud na Leah Aroun kwa nyakati tofauti walitoa ushuhuda wa mabadiliko ya ufahamu wa mambo kwa watoto wao ,ambao kwa sasa kabla ya kula na kulala lazima waombe na wanafanya vizuri darasani na kulishukuru kanisa hilo kwa kutoa huduma ya watoto bila kujali itikadi za dini.

Kwa upande wa watoto Leticia Barnabas na Azizi Ally  wakiri kupata marifa ya kiroho na wmepata mwanga wa ndoto zao siku zijazo na kuwasihi wazazi na walezi wamwamini mungu kwa ibada za kweli,wasimwasi mungu kwa kukiuka maadili mema na kuzifurahia zawadi walizopewa na wafadhili wao kama sabuni na biskuts.

Naye Mchungaji wa AICT wa hapao aliwaasa walezi na wazazi walee watoto katika uchamungu,upendo,imani ambayo itampa mwelekeo wa maadili mema siku za usoni kwa kusaidia watoto wenye uhitaji ,ambapo kupitia ufadhili wa shirika la Compassion linajivunia kuwa na  vijana wengi wenye uchumi mzuri katika maisha yao,ambapo wengine leo wanashika nyadhifa kubwa serikalini .
Mwisho.

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages