Na Ally Daud -MAELEZO
MAKAMU wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anatarajia
kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Mpango wa Taifa wa Miaka Mitano
(2017-22) wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.
Hayo
yamesemwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto (Maendeleo ya Jamii) Bi. Siaba Nkinga katika
mkutano na waandishi wa habari, ambapo alisema uzinduzi huo unatarajia
kufanyika Desemba 13 mwaka huu Jijini Dar es Salaam
“Mpango
huu jumuishi wa miaka mitano utakaouzinduliwa umezingatia nguzo kuu
mbili, ambazo ni kuzuia na utoaji wa huduma kwa wahanga wa vitendo vya
ukatili wa kijinsia” alisema Bi. Nkinga
Alisema
kuwa mpango kazi huo unatarajiwa kutoa msukumo mpya katika kuwezesha
utekelezaji majukumu ikiwemo kutetea, kushauri na kutoa elimu kwa umma
ili kuongeza uelewa kwa jamii kuhusu athari za ukatili kwa wanawake.
Kwa
mujibu wa Nkinga alisema kuwa utafiti uliofanywa na Shirika la
Kuhudumia Watoto Ulimwenguni (UNICEF) wa mwaka 2015, unaonyesha kuwa
Tanzania ina asilimia 3.5 ya watoto wa umri wa miaka 7 – 17 walio nje
ya shule kutokana na sababu mbalimbali za ukatili.
Alibainisha
Vitendo vya ukatili wa kijinsia vilivyoshamiri zaidi ni pamoja na
vipigo, ubakaji, ulawiti, mauaji ya vikongwe, na watu wenye ualibino,
usafirishaji haramu wa binadamu, kutelekeza familia, udhalilishaji,
ukeketaji, mimba na ndoa za utotoni.(P.T)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269