Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohamed akiwa katika pozi
Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohammed akimwaga tabasamu la furaha wakati wa shughuli yake ya kuagwa (kitchen mada) iliyofanyika Sinza Mapambano, Dar es Salaam jana, tayari kwa leo Ijumaa, Desemba 23, 2016 akijaaliwa atafunga ndoa na mwandani wake. Inshaallah tumtakie kila la Kheri.
Ni
hivi punde Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohamed (wa tano kulia)
atafunga Ndoa yake na mpendwa wake Ashrafu Issa, hapa akiwa katika
picha ya pamoja wanafamilia
Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohamed akiingizwa katika ukumbini wakati wa
shughuli yake ya kuagwa (kitchen mada) eneo la Sinza Mapambano Dar es
Salaam
Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohamed akitunzwa na mmoja wa mwanafamilia
Kikundi
cha kinamama wakitumbuiza kwa dufu wakati wa hafla ya kumuaga Bi Harusi mtarajiwa, Amina Mohamed iliyofanyika nyumbani kwao
Sinza Mapambano, Dar es Salaam
Mmoja wa mwanafamilia akimtuza zuria la kufutia miguu
Bi Harusi mtarajiwa, Amina Mohamed katika pozi na
Muuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhumbili ambaye ni wifi yake mtarajiwa, Subira Mheta.
Amina Mohamed (kushoto) akiondoka ukumbini tayari kwa
kujiandaa na hafla ya Harusi yake itakayo fanyika leo baada ya Swala ya
Ijumaa nyumbani kwao Sinza Mapambano Dar es Salaam
Wana kikundi cha Upendo Group wakimtunza Amina Mohamed (wanne kushoto) ambapo ni wanakikundi
wenzake na Wifi yake, Subira Mheta ambaye ni Muuguzi Hospitali ya
Taifa Muhimbili. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA wa Kampuni ya K M Express
Photo Studio na Mmiliki wa ujijirahaa blog
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269