Lionel Messi ametana na Murtaza Ahmadi mvulana raia wa Afghanistani bingwa wa kuvaa jezi ya plastic
Mtoto
huyo wa kiume mwenye umri wa miaka 6 kapata umaarufu mkubwa sana katika
tovuti mbalimbali na mitandao ya kijamii kutokana na kitendo chake cha
kuvaa jezi ya mfumko wa plastic wenye ranfgi ya bendera ya nchi ya
Argentina.Jana mtoto Murtaza Ahmadi amekutana mtu anaemwona kama “role
model” wake au shujaa wake anaetaka kufuata nyayo zake.
Mchezaji
soka huyo wa klabu ya Catalonia amekutana na Murtaza katika uwanja wa
mpira wa miguu huko Doha, nchi Qatar wakati wa mechi kati ya Al-Ahli ya
Saudi Arabia na Barcelona bingwa mtetezi wa La Liga nchini Hispania.
Katika mchezo huo Al-Ahil alipigwa bao 5 na mabingwa hao wa Hispania
licha ya wao kupata goli 3.
Kwa mara
ya kwanza kamera zilimpata Murtaza mwezi Januari mwaka huu akiwa amevaa
mfuko wa rangi ya blue na nyeupe na nyuma ya jezi kukikiwa na namba 10
iliyoandikwa kwa wino wa kalamu ya kawaida huko Kabul nchi Afganistani.
Miezi 11 baadae, picha ya shujaa wa Murtaza imekuwa kitu halisi. Jana
Murtaza amekuana na Messi na kuingia nae mpaka katikati ya uwanja.
Ikumbukwe
pia mtoto Murtaza, mwezi mmoa tu baada ya kuvaa mfuko wa jezi ya
Argentina, shirika la Umoja wa Mataifa linalojihusisha kukusanya fedha
kwa ajili ya watoto lilimzawadia “tshirt” halisi yenye saini ya shujaa
huyo wa soka Baba wa mtoto huyo anaefahamika kama Muhammad Arif Ahmadi,
alizungumza na kituo cha television cha CNN kuwa mwanae alipopata jezi
ya Messi, alijona mwenye furaha kubwa sana maishani.
Mimi nawe
tunaoishi katika dunia kijiji, tuna ndoto gani ya kuifanya furaha yetu
iwe kitu halisi. Dr. Martin Luther King Jr, alisema anayo ndoto. Mahatma
Gandhi kiongozi wa mapinduzi na uhuru wa India aliamini katika ndoto ya
kuwaunganisha Wahindu kupinga ukoloni wa Uingereza bila kutumia nguvu,
vurugu au vitendo vya kihalifu.
Mtoto wa
miaka 6 kaonesha ndoto yake bila aibu na miezi 11 baadae amekutana na
shujaa wake kwa kusimama nae uwanjani mbele ya mamilioni ya watu duniani
kote walioweza kushuhudia tukio hili.
Ndugu yangu unaesoma makala hii, bado hujachelewa, weka ndoto yako kwa kuwashirisha watu wajue nini unataka kuufanyia ulimwengu.
Ipo siku kuna mtu utakutana nae anaeweza kujenga daraja la wewe kufikia ndoto yako.
Ipo siku kuna mtu utakutana nae anaeweza kujenga daraja la wewe kufikia ndoto yako.
Kama una
ndoto washirikishe wengi wajue nini unataka kufanya. Kuna ambao
watakucheka, kuna ambao watakubeza, ila kuna siku utakutana na mtu
anaeweza kuwa sehemu ya ndoto na furaha yako kutimia.
Jenerali Colin Powell ambae alipata kuwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani alipata kusema,
“A dream doesn't become reality through magic; it takes sweat, determination and hard work”
Ndoto haitokei kuwa halisi kwa njia ya miujiza, inahitaji kutoa jasho, kudhamiria na kufanya kazi kwa juhudi.
“A dream doesn't become reality through magic; it takes sweat, determination and hard work”
Ndoto haitokei kuwa halisi kwa njia ya miujiza, inahitaji kutoa jasho, kudhamiria na kufanya kazi kwa juhudi.
Mtoto wa
miaka 6 aliweka ndoto kwa matendo kwa kuchukua mfuko wa plastic, akavaa
na kujitokeza hadharani bila kujali aibu au hatari za vita huko Kabul,
Afghanistan.
Wewe
msomaji wangu, unaona fursa gani, unachukua hatua gani ya kimkakati ili
kufikia malengo yako. Je, ni aibu, maneno ya watu au watu watakuonaje
ukichukua hatua ya kwanza kupiga hatua kuelekea kwenye ndoto ya furaja
maishani mwako?
Dk. A. R.
Bernard mmmoja wa viongozi wa dini katika wa New York alipata kusema
mafaniko ya mtu ni jumla ya maamuzi anayofanya kwa kujua au kutokujua
katika maisha yake juu ya sayari dunia.
Nakutakia siku njema.
Nakutakia siku njema.
Fredrick Matuja
fmatuja@hotmail.com(P.T)
fmatuja@hotmail.com(P.T)
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269