Wafanyabishara wa vyuma chakavu wamedaiwa kuihujumu miunodmbinu ya Kampuni ya TTCL mkoani Kigoma hali na kuisababishia kampuni hiyo hasara ya zaidi ya Sh. Milioni 650.
Akizungumza jana mjini Ujiji mkoani hapa, Meneja wa shirika hilo Robert Miala, alisema
wafanyabiashara hao wamekuwa chanzo cha kuharibiwa kwa miundombinu ya shirika
hali inayoathiri utendaji kazi kwa wateja wake, na kwamba baadhi ya maeneo yaliyoadhirika sana na kutokana na uharibifu huo wa miundombinu katika wilaya ya kigoma
mjini katika kata ya Gungu ambayo kwa sasa haina mawasiliano
kabisa.
Alieleza kuwa, kitendo cha kuhujumu miundombinu ya mali za
umma ni janga kwa taifa kuimarika kwa uchumi, ingawa wezi wa miundombinu hiyo wanahisi
wanaondoakana na umaskini wa kipato lakini watambue serikali inaingia gharama kubwa
katika kukarabati upya maeneo yaliyoharibiwa ambazo wengi huiba kwa ajili ya
kupata madini ya kopa yaliyomo kwenye nyaya hizo.
Miala alisema katika
mkoa wa kigoma eneo ambalo ni salama ni wilaya ya Kibondo tu,huku kigoma mjini
na kasulu ni vinara wa kuhujumu miundombinu ya TTCL hali inayowapa changamoto
katika kurudisha huduma kwa wateja,ambao wengi wao ni mashirika ya umma na
sekta binafsi wenye uhitaji wa huduma hiyo.
“wizi huu ni wa muda mrefu,nimeukuta lakini fedha nyingi
zimepotea katika hili,na tunarudisha huduma kwa kile tunachopata ili wadau wetu
muhimu wasikose huduma yetu,lakini wandishi tusaidieni kuelimisha umma,kuwa
wizi wa miundombinu ya mawasiliano ya serikali ni kosa la uhujumu
uchumi,tumeshirikisha jeshi la polisi ili wahalifu watiwe nguvuni” alifafanua
Meneja huyo.
Alipohojiwa hilo Kamanda wa Polisi Kigoma Ferdinand Mtui
akiri kupokea malalamiko toka kwa shirika hilo na Desemba,20,mwaka huu saa 8.45
mchana eneo la Rose Corner Manispaa ya
kigoma Ujiji wilayani kigoma walifanikiwa kuwakamata wafanyabiahshara watatu wa chuma chakavu wakiwa na kilo 12 za
nyaya za TTCL ambazo tayari zilichubuliwa
gamba na kuzificha ndani ya pipa la chuma.
Kamanda huyo alisema watuhumiwa wote ni wakazi wa mwanga
manispaa ya kigoma ujiji na watafikishwa mahakamani pindi uchunguzi
utakapokamilika na kutoa rai kwa jamii watambue umuhimu na faida ya kutunza miundombinu
ya taifa ni moja ya kuwafichua wahalifu wanaohujumu uchumi wa taifa,ili
wachukuliwe hatua za kisheria na iwe funzo kwa wengine.
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269