Breaking News

Your Ad Spot

Dec 17, 2016

TANZANIA NA KENYA ZASAINI MAKUBALIANO YA TUME YA PAMOJA YA USHIRILIANO

kashim
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Balozi Dkt. Augustine Mahiga kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Mhe. Balozi Dkt. Amina Mohammed wakisaini Makubaliano ya Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya.  Makubaliano hayo yamesainiwa kufuatia Kikao cha Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JCC) kati ya Tanzania na Kenya kilichofanyika tarehe 1 hadi 3 Desemba, 2016 ambapo masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya nchi hizi mbili yalijadiliwa na kukubaliwa. Masuala ya ushirikiano ni pamoja na kilimo, uchukuzi, utalii, nishati na madini na uvuvi. Hafla hiyo fupi ya uwekaji saini makubaliano hayo imefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini  Dar es Salaam tarehe 16 Desemba, 2016.
Waziri Mahiga na Waziri Mohammed wakibadilishana makubaliano hayo mara baada ya kusaini.
Waziri Mahiga akizungumza katika hafla hiyo.Katika hotuba yake Mhe. Mahiga alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana kwa karibu na Kenya na kwamba makubaliano yaliyosainiwa yataimarisha mahusiano hayo kwa kuboresha mazingira ya uwekezaji, kurahisisha ufanyaji biashara na kuongeza fursa za ajira kwa vijana wa nchi hizi mbili.
Waziri Amina naye  akizungumza kwenye hafla hiyo. Katika hotuba yake aliahidi Kenya kuendelea kushirikiana na Tanzania kwa karibu katika masuala yote yaliyokubaliwa.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi akitoa neno la shukrani katika hafla hiyo ya uwekaji saini Makubaliano ya Tume ya Pamoja ya Ushirikiano
Sehemu ya wajumbe kutoka Kenya waliohudhuria  hafla ya uwekwaji saini wa Makubaliano ya Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya.  Kulia ni Balozi wa Kenya nchini Tanzania, Mhe. Chirau Ali Mwakwere
Sehemu ya ujumbe wa Tanzania nao wakishuhudia uwekwaji  saini katika makubaliano ya tume ya pamoja ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya. Kushoto ni Balozi Samwel Shelukindo, Mkurugenzi wa Idara ya Afrika akifuatiwa na Bw. Stephen Mbundi, Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Masahriki
Mshereheshaji ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga akiwakaribisha wageni wakati wa hafla ya uwekaji saini Makubaliano ya Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya.
Sehemu ya maafisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Waandishi wa Habari waliohudhuria  hafla hiyo.
Picha ya Pamoja(P.T)

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages