Rais
mteule wa Marekani Donald Trump ,amesema kuwa Marekani inafaa kuiomba
China kuiweka manuwari ya Marekani iliopatikana katika bahari ya kusini
mwa taifa hilo.
Awali Trump alikuwa ameishutumu Beijing kwa kuiba manuwari hiyo katika maji ya kimataifa.
China
iliichukua manuwari hiyo katika pwani ya Ufilipino wakati meli za
wanamaji wa Marekani zilipojaribu kuichukua, hatua ilioikasirisha
Marekani.
Beijing imesema kuwa itaikabidhi Marekani, lakini matamshi ya Trump huenda yakatatiza mpango huo.
Hii ni mara ya tatu katika wiki kadhaa kwa yeye kukosana na China.
Wakati
huohuo Trump amekamilisha ziara yake ya wiki tatu ya kusherehekea
ushindi , katika mji ulioshuhudia mkutano mkubwa zaidi wakati wa kampeni
zake.
Alipowasili
katika mji wa Mobile, Alabama, Trump alikaribishwa na kundi la wanawake
waliovalia mavazi ya kitamaduni yanayovaliwa na jamii za kusini mwa
Marekani.
Katika uwanja uliojaa pomoni, Trump aliahidi kwamba atatimiza ahadi yake ya kujenga ukuta kwenye mpaka wa Mexico na Marekani.
Trump ataapishwa tarehe 20 mwezi Januari.BBC
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269