Donald
Trump ametoa shutuma mpya kupinga madai ya ujasusi nchini Marekania kuwa
wadukuzi nchini Urusi waliingilia uchaguzi wa Marekani.
Rais huyo
mteule wa Marekani pia aliuliza kuhusu ni kwa nini madai hayo ya
udukuzi hayakutolewa kwa umma kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.
"Kabla
wadukuzi hawajakamatwa kwenye kitendo, ni vigumu sana kubaini ni nani
alikuwa akidukua. Mbona hili halikusemwa kabla ya uchaguzi?" Trump
aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter leo Jumatatu.
Siku ya
Ijumaa maafisa wa CIA walivyambia vyombo vya habari nchini Marekani
kuwa, wadukuzi wa Urusi walijaribu kuvuruga uchaguzi na kumpendelea
Trump.
Timu ya ilijibu madai hayo na kusema: "Hawa ni sawa na wale watu waliosema kuwa Saddam Hussein alikuwa na silaha za maangamizi."
Trump
yuko nyuma ya Trump katika wingi wa kura kwa karibu kura milioni 2.8
licha ya yeye kushinda kwa kura nyingi zaidi za wajumbe katika historia
ya Marekani.BBC
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269