Breaking News

Your Ad Spot

Dec 18, 2016

UN KUPIGIA KURA AZIMIO LA KUWAPELEKA WACHUNGUZI ALEPPO

USA UN-Sicherheitsrat tagt in New York zu Syrien (Getty Images/AFP/D. Reuter)
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kupiga kura leo Jumapili (18.12.2016) kuwatuma wachunguzi Aleppo,wakati raia na waasi waliokwama wanasubiri kuanza tena zoezi la kuwaondowa kutoka Aleppo.
Wawakilishi  wa  waasi  wameliambia  shirika  la  habari  la Ufaransa AFP makubaliano  yalifikiwa  kuruhusu  watu  wengi  zaidi kuondoka  katika  eneo  hilo ambalo  limeharibiwa kutokana  na mapigano  mabaya  kabisa  kutokea  katika  vita vya  miaka  sita sasa  ambavyo  vimewauwa  zaidi  ya  watu 310,000. Lakini  hakuna uthibitisho  kutoka  utawala  wa  rais Bashar al-Assad  ama washirika wake  wakubwa Urusi  na  Iran, ambao  wako  katika mbinyo  mkubwa  wa  kimataifa  kufikisha  mwisho  kile rais Barack Obama  anachoshutumu  kuwa ni "hali  ya  kuogofya" mjini  Aleppo.
Baraza  la  Usalama  la  Umoja  wa  mataifa  linatarajiwa  kuketi mchana  leo  Jumapili  kupigia  kura pendekezo  la  Ufaransa la kuwapeleka  waangalizi  wataoasimamia  zoezi  la  kuwaondoa   watu na  wataripoti  kuhusu ulinzi  wa  raia, lakini  pendekezo  hilo linakabiliwa  na  upinzani  kutoka  kwa  Urusi  ambayo  ina  kura  ya turufu.
Balozi  wa  Ufaransa Francois Delattre  amesema  kuwapo  kwa kikosi  cha  jumuiya  ya  kimataifa  kutazuwia  Aleppo  kugeuka  kuwa Srebrenica, ambako  maelfu  ya  Wabosnia  wanaume  na  vijana waliuwawa mwaka  1995  wakati  mji  huo  ulipokamatwa  na majeshi  ya  Waserbia  wa  Bosnia wakati  wa  vita  vya  Balkan .
"Lengo  letu  kwa  mswada  huu  wa  azimio  ni  kugeuka  kitu  kingine kama  Srebrenica  katika  awamu  hii  haraka  kufuatia  operesheni za  kijeshi," Delattre  ameliambia  shirika  la  habari  la  AFP. Familia zililala  nje  usiku  kucha  katika  baridi  kali  katika   majengo ambayo  yameharibiwa  kwa  mabomu  katika  wilaya  ya  Al-Amiriyah  mjini  Aleppo, eneo  ambalo  ndio linatumika  kuwaondoa watu  kabla  ya   zoezi  hilo  kusitishwa  siku  ya  Ijumaa, ameripoti mwandishi  wa  habari  wa  AFP. Abu Omar  amesema  baada  ya kusubiri  nje  katika  baridi  kali  kwa  masaa  tisa  siku  iliyopita, amerejea  Jumamosi  na  kuambiwa  kwamba  mabasi  hayatakuja kuwaondoa.
Hali  ya  chakula  ni  mbaya
"Hakuna  chakula  tena  ama  maji  ya  kunywa, na  hali inaendelea kuwa  mbaya  kila  siku," amesema, na  kuongeza  kwamba  watoto wake  wanne  ni  wagonjwa kutokana  na  baridi.
Dazeni  kadhaa  za  malori  yakiwa  na  msaada  wa  kiutu  yalivuka mpaka  wa  Uturuki  siku  ya  Jumamosi kuingia  Syria , na  kuweka misaada  hiyo  katika  maeneo  salama  yaliyotengwa.
Serikali  inawalaumu  waasi  kwa  kusitishwa  kwa  zoezi  hilo  la kuondolewa  ambalo  lilianza  siku  ya  Alhamis, ikisema  walijaribu kupitishwa  kwa  magendo  silaha  nzito  na mateka. Upinzani unaishutumu  serikali  kwa  kusitisha  zoezi  hilo kujaribu  kupata kuondolewa  kwa  wakaazi  kutoka  Fuaa  na  Kafraya, vijiji  viwili vilivyoko  chini  ya  mzingiro  wa  waasi  katika  miji  ya  Madaya  na Zabadani  katika  jimbo  la  Damascus  ambayo imezingirwa na majeshi  ya  serikali.
Al-Farook Abu Bakr, kutoka  kundi  lenye msimamo  mkali  la  waasi la  Ahrar al-Sham, amesema  makubaliano  yalifikiwa  kwa  ajili  ya kuanza  tena  kuwaondoa   raia.
"Kutakuwa  na  uondoaji  wa  watu  kutoka  Fuaa  na  Kafraya , pamoja  na  Madaya  na  Zabadani , na  wakaazi  wote  wa  Aleppo na  wapiganaji  wataondoka," amesema. Lakini  serikali  haijatangaza makubaliano  yoyote. Mjumbe  wa  Umoja  wa  Mataifa  Staffan de Mistura  anakadiria  kwamba  kuanzia  Alhamis  raia 40,000  na huenda  zaidi  ya  wapiganaji  wapatao 5,000 bado  wanaendelea kuwapo katika  eneo  la  Aleppo  mashariki. Afisa  wa  Uturuki amesema  watu  90  waliojeruhiwa  kutoka  Aleppo  waliingia  Uturuki kwa  ajili  ya  matibabu  tangu  siku  ya  Alhamis.DW

No comments:

Post a Comment

Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269

Post Top Ad

Your Ad Spot

Pages