Baraza la
Usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kupiga kura leo Jumapili
(18.12.2016) kuwatuma wachunguzi Aleppo,wakati raia na waasi waliokwama
wanasubiri kuanza tena zoezi la kuwaondowa kutoka Aleppo.
Wawakilishi
wa waasi wameliambia shirika la habari la Ufaransa AFP
makubaliano yalifikiwa kuruhusu watu wengi zaidi kuondoka katika
eneo hilo ambalo limeharibiwa kutokana na mapigano mabaya kabisa
kutokea katika vita vya miaka sita sasa ambavyo vimewauwa zaidi
ya watu 310,000. Lakini hakuna uthibitisho kutoka utawala wa rais
Bashar al-Assad ama washirika wake wakubwa Urusi na Iran, ambao
wako katika mbinyo mkubwa wa kimataifa kufikisha mwisho kile rais
Barack Obama anachoshutumu kuwa ni "hali ya kuogofya" mjini
Aleppo.
Baraza
la Usalama la Umoja wa mataifa linatarajiwa kuketi mchana leo
Jumapili kupigia kura pendekezo la Ufaransa la kuwapeleka
waangalizi wataoasimamia zoezi la kuwaondoa watu na wataripoti
kuhusu ulinzi wa raia, lakini pendekezo hilo linakabiliwa na
upinzani kutoka kwa Urusi ambayo ina kura ya turufu.
Balozi
wa Ufaransa Francois Delattre amesema kuwapo kwa kikosi cha
jumuiya ya kimataifa kutazuwia Aleppo kugeuka kuwa Srebrenica,
ambako maelfu ya Wabosnia wanaume na vijana waliuwawa mwaka 1995
wakati mji huo ulipokamatwa na majeshi ya Waserbia wa Bosnia
wakati wa vita vya Balkan .
"Lengo
letu kwa mswada huu wa azimio ni kugeuka kitu kingine kama
Srebrenica katika awamu hii haraka kufuatia operesheni za
kijeshi," Delattre ameliambia shirika la habari la AFP. Familia
zililala nje usiku kucha katika baridi kali katika majengo
ambayo yameharibiwa kwa mabomu katika wilaya ya Al-Amiriyah
mjini Aleppo, eneo ambalo ndio linatumika kuwaondoa watu kabla
ya zoezi hilo kusitishwa siku ya Ijumaa, ameripoti mwandishi wa
habari wa AFP. Abu Omar amesema baada ya kusubiri nje katika
baridi kali kwa masaa tisa siku iliyopita, amerejea Jumamosi na
kuambiwa kwamba mabasi hayatakuja kuwaondoa.
Hali ya chakula ni mbaya
"Hakuna
chakula tena ama maji ya kunywa, na hali inaendelea kuwa mbaya
kila siku," amesema, na kuongeza kwamba watoto wake wanne ni
wagonjwa kutokana na baridi.
Dazeni
kadhaa za malori yakiwa na msaada wa kiutu yalivuka mpaka wa
Uturuki siku ya Jumamosi kuingia Syria , na kuweka misaada hiyo
katika maeneo salama yaliyotengwa.
Serikali
inawalaumu waasi kwa kusitishwa kwa zoezi hilo la kuondolewa
ambalo lilianza siku ya Alhamis, ikisema walijaribu kupitishwa
kwa magendo silaha nzito na mateka. Upinzani unaishutumu serikali
kwa kusitisha zoezi hilo kujaribu kupata kuondolewa kwa wakaazi
kutoka Fuaa na Kafraya, vijiji viwili vilivyoko chini ya
mzingiro wa waasi katika miji ya Madaya na Zabadani katika
jimbo la Damascus ambayo imezingirwa na majeshi ya serikali.
Al-Farook
Abu Bakr, kutoka kundi lenye msimamo mkali la waasi la Ahrar
al-Sham, amesema makubaliano yalifikiwa kwa ajili ya kuanza tena
kuwaondoa raia.
"Kutakuwa
na uondoaji wa watu kutoka Fuaa na Kafraya , pamoja na Madaya
na Zabadani , na wakaazi wote wa Aleppo na wapiganaji
wataondoka," amesema. Lakini serikali haijatangaza makubaliano
yoyote. Mjumbe wa Umoja wa Mataifa Staffan de Mistura anakadiria
kwamba kuanzia Alhamis raia 40,000 na huenda zaidi ya wapiganaji
wapatao 5,000 bado wanaendelea kuwapo katika eneo la Aleppo
mashariki. Afisa wa Uturuki amesema watu 90 waliojeruhiwa kutoka
Aleppo waliingia Uturuki kwa ajili ya matibabu tangu siku ya
Alhamis.DW
No comments:
Post a Comment
Toa Maoni kistaarab kwa Hoja kwa faida ya wenzako. au tundikie kupitia nkoromo@gmail.com, simu 0672223269